Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Sunday, November 25, 2018

Je wajua Sifa za Mwanamke wa Kuoa?


Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.

Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachowezakuwafanya wakapata wachumba niuzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.

Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa.

Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

1. MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake.

Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingiutamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.

Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.

Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.

Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.

2. WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja sualana kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa anatabia mbaya.
Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.

Si hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.

3. WENYE UCHU NA MAENDELEO
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani 'golikipa'. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini.

Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.

4. WASIOPENDA MAKUU
Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia "leo tunakwenda wapi dear?"

Akimuona rafiki yake kanunua simuya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia,"mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’

Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.

Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leoamemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.

Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitajiupo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulaniwakati inawezekana uwezekano haupo.

5. WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.

Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotokea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?

Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.

Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.

Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.
Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali

Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

Namna Ya Kuishi Na Watu Wenye Tabia Ngumu


Ni ngumu na kamwe siyo rahisi kumbadilisha mtu mwenye tabia ngumu awe rafiki. Badiliko hili lawezekana ikiwa mhusika (mwenye tabia ngumu) atadhamiria na kuwatayari kushughulika ili kubadilika.

Kwa hiyo kama ni ngumu au haiwezekani kumbadilisha basi jaribu kubadili mtazamo wako na jinsi unavyoishi naye au nao, kwasababu mara nyingi wewe ndiye unaye kwazika au kuumizwa wakati yeye (yule anayekuudhi) anafanikiwa na anaendelea na furaha yake tu.

Mawasiliano baina yetu na watu wengine yanajumuisha jinsi tunavyowafanyia wengine na jinsi wao wanavyotufanyia sisi (reaction and counter reaction). Kwa kubadili jinsi sisi tunavyowatendea wengine inaweza kubadili jinsi wao wanavyotutendea sisi. Hata kama ni kwa muda au kitambo kidogo tu. Hata kama hali hii haibadili hali kwa kudumu ila inaweza kurahisisha mazingira ya kuishi na mtu au watu wenye tabia ngumu.

Kila wakati lazima uwe na akili sana katika kuishi na watu wenye tabia ngumu, kama hutoweza kujizuia, na ukaanza kuwabwatukia basi itakuwa unaleta tatizo hasa pale ambapo mwenye tabia hii ngumu ni bosi wako. Je, utaropoka au kutukana kama ulivyozoea?
Hata kama mtu au watu wenyetabia hii wako ndani ya familia na yamkini ni wadogo kwako kiumri, bado kuropoka na kuwapayukia siyo suluhisho, hali hii yaweza kukugharimu.

Najua kila mmoja wetu anajinsi anavyofanya kwa mtu au watu wenye tabia ngumu. Wote hatuna namna moja, mmoja anaweza kuwa ni mkimya na mwenye ujasiri hata anapoudhiwa, mwingine hupayuka na kumjibu yule anaye muudhi, mwingine anaamua kulia tu anapoudhiwa, wako wanaozira na kuamua kutozungumza tena na aliyewaudhi, wapo ambao husambaza habari mbaya kuhusu huyo mwenye maudhi, wako ambao huamua kumwambia uso kwa uso jinsi walivyo kwazika, sijui staili yako ni ipi.

Ni rahisi sana kuumizwa au kuudhiwa na maneno au matendo ya mwingine, na mara mtu huyo anapojua kuwa unaumia yeye hupata nguvu, hii huwa ndiyo silaha yake muhimu pale mnapopambana.

Unachotakiwa kufanya ni kuwaachia wakati wote wao wawe washindi, kamwe usitafute kushindana nao, utaumia mwenyewe. Njia pekee ni kujitahidi kuwa mjanja na mwenye akili kuliko yeye na pia kuwa na ushawishi katika yale wanayotaka kuyatenda hata pasipo wao kugundua.
Je, unawajibu vipi watu hawa (How do you react?)
Ni jambo jema kuanza kujitazama jinsi unavyowatendea wengine na jinsi tunavyoshughulika na wale wanaotukwaza. Kumbuka kuwa jinsi unavyoikabili hali hiyo katika mazingira fulani inawezekana isiwe hivyo katika mazingira mengine.

Watu wenye tabia ngumu na zinazotatiza mara nyingi huweka mitego ya maneno au matendo na kwa kiasi kikubwa unaweza kunaswa na kuwaruhusu wakuchezee jinsi watakavyo, na kati ya vitu wanavyo vipenda na kuvitamani ni kukuona unalia na kuumia na kuchanganyikiwa. Kwahiyo fikiri kwanza kabla hujafanya chochote mbele yao.

Watu watabia hii mara zote huwachukulia na kuwatendea watu wote sawa kwa hiyo usifikiri kila alichosema au alichofanya kwako ni cha kibinafsi sana na alikikusudia kwako. Angeweza kufanya au kusema hivyo hivyo hata kwa mwingine aliye karibu naye wakati ule. Kwa kufahamu hili itakusaidia kupunguza maumivu yanayoletwa na hisia zako kwake.

Hembu jiulize ni jinsi gani umewahi kukabiliana na mtu au watu wa jinsi hii, na je ilikuwa ni kwa jinsi ya kuumiza au kuelemisha? Fahamu kwamba kujibu kwa kupayuka, kutukana au kubishana haisaidii, bali kunakushusha chini ya miguu ya yule aliye kusababishia maumivu hayo, na sasa atakuwa anafurahia na kukuona wewe mjinga.

Ni chaguo lako, la ni jinsi gani utakabiliana na mtu au watu wa aina hii, ingawa unaweza kuchagua njia bora itakayoweza kukusaidia kukuimarisha na kupunguza udhaifu wako, zaidi ya kuamua kuchagua njia ambayo itakuacha umeumia, umechoka, umekatishwa tamaa na umejeruhika moyo.

Hii haimaanishi uwe mtu wa kusema ndiyo tu kwa kila kitu na kila mtu, na haimaanishi kuwa hutakiwi kukasirika HAPANA, hasira ni asili na haina tatizo lolote hapa, ila tu matokeo ya hasira hiyo ndiyo yanayoweza kuleta shida. Je ni jinsi gani unakabiliana na hasira yako na unaionyeshaje? Kwa fujo, kupayuka kubishana, kulia, kuvunja vitu, kunyamaza n.k.

Ili Kujua jinsi watu wenye tabia ngumu wanavyokuathiri. Jiulize maswali yafuatayo:
Je, ni unataka kutawaliwa na wengine?
Najua jibu ni kwamba hakuna nayetaka kutawaliwa na mwingine, na ndiyo maana unaweza kujikuta unabishana au kushindana na huyo anaye kukwaza.

Tatizo ni kwamba mwisho wewe ndiyo unaumia na yeye anabaki kufurahia kwa kukushinda mfano; tazama fujo za madereva barabarani hususan wale wa daladala.
Nikweli unahasira naye, lakini je hiyo ni njia muafaka ya kumkabili? kumbuka mwishoni atakayeumia ni wewe.

Fikiri kama unatatizo la shinikizo la damu kama utakubali kuyumbishwa kihisia na tabia mbovu za mwingine wewe ndiyo utabaki unaumia na siyo tu kama hutoweza kufanya vile moyo wako utakavyo bali pia utaachwa ukijihisi kuchoka, kuumizwa kwa hisia zako mwenyewe na kukatishwa tamaa na tabia yako wewe mwenyewe.

Nini Mwitikio wako pale unapoudhiwa? (Haswa na yule mwenye hasira na wewe)
Je, unalipa hasira kwa hasira?
Je, unajitetea na kuukimbia ukweli (being defensive)
Au unajificha kutoroka au kumkwepa?
Njia zote hizi hapa juu siyo nzuri.

Hata kama una haki ya kukasirika, lakini bado atakayeumia unabaki kuwa ni wewe. Na siyo tu utaumizwa na kukasirishwa kwa tabia yake mwenye kukuudhi bali utaumizwa moyoni mwako kwa vile wewe ulivyotenda, dhamiri itakushtaki zaidi (guilty conscious).

Je, unajizumgumziaje wewe mwenyewe, vibaya au vyema?
Mfano: Ukweli mimi najichukia haswa ninapofikia kipindi cha mitihani au usaili.
Hivi mimi nikoje?
Hivi kwa nini nimeumbwa hivi?
Kamwe mimi siwezi kufanya lolote jema!
Wakati wote mimi ni mtu wa bahati mbaya tu!

Wala huhitaji kujichukia unapofikia wakati wa mitihani au usaili, unachohitaji kufanya ni kujiandaa mwenyewe vizuri na kuwahi mapema katika eneo la tukio.
Hisia potofu na zisizojenga ambazo tunajiwazia wenyewe mara nyingi hutupotezea muda na mara tunapoziruhusu hutuharibia siku yetu nzima.

Unafanya nini unapopingwa? (what do you do when you are criticized)
Wako watu wanaopendelea kupinga wengine katika kila kitu, hata katika vile visivyostahili kupingwa,hakuna chochote chema kinachoweza kusemwa na yeyote, bali yeye peke yake. Hata kama kilichosemwa kina ukweli kwa asilimia kubwa basi mtu huyu atajitahidi walau kurekebisha hata lugha tu, ili mradi kisipite hivihivi bila yeye kukipinga japo kidogo (hawa ndiyo wale wenye tabia ngumu).

Hali hii huwapa kufurahi na kujijengea nguvu kwa jinsi wanavyopinga wengine.
Ni kweli upinzani mwingine ni wa ukweli na unajenga lakini hapa nakazia wale wanaopinga ili tu kujifurahisha nafsi zao na kuwafanya wale wanaowapinga waumie mioyo.

Je, unapopigwa, unajibuje? Je, unajitetea au unajishusha na kukubali kila kinachopingwa kwa kuamini kwamba anayekupinga yuko sawa na kwa hiyo unayameza maoni yako yote, bila kuchambua kwa kina mapingamizi hayo.

Kuna jinsi ambavyo unaweza kumkabili au kumjibu anayekupinga na ikawa kama umeweka petroli kwenye moto, upinzani utawaka na hata kuleta ugomvi, lakini pia iko njia ambayo unaweza kumjibu mtu huyu na ukanyamazisha fukuto lote.

Je, una mtazamo hasi (mtazamo usiofaa) na wa kudumu katika kitu fulani?
Mfano; Labda unasema “Mambo yangu hayaendelei tangu nihamie katika nyumba hii, au mambo yangu yanakwama tangu nimuoe au niolewe na huyu, ni matatizo tu tangu tuoane, watoto hawa hasara tupu.” n.k.

Mtazamo huu hasi, waweza kukugharimu siyo tu kukunyima raha bali pia waweza kuharibu hisia zako na za wengine pia.
Ukijikuta katika hali hii ni vyema kujifahamu na kujitahidi kuelewa nini tatizo husika na jitahidi kubadilisha mtazamo wako.

Tafuta vile vitu ambavyo unaweza kuvitazama katika mtazamo chanya hata kama ni vidogo. Tafuta kuviongelea vile unavyovipenda zaidi ya vile usivyovipenda.
Je, unazimeza hisia zako zote, nzuri na mbaya?

Je, unaona ni ngumu sana kusema “nakupenda” “umependeza” “umeniudhi” n.k. labda unaweza kusema neno moja tu na siyo lingine. Wengi wetu tumekuzwa katika mazingira ambayo tunahofu kusema chochote ili tu tusije tukamkwaza mtu, hata kama tunaumizwa au tunajisikia vyema kusema kitu fulani, lakini tunajizuia.

Badala yake tunakwenda kusemea pembeni. Yamkini kunyamaza kunaweza kuwa na faida katika baadhi ya mazingira lakini siyo hata katika kukubali vitu visivyofaa. Hakuna ubaya wowote katika kuelezea jinsi unavyojisikia moyoni mwako ili mradi tu unaeleza kila unachokihisi kwa hali njema na siyo kwa hasira au shari. Katika hali hii kamwe hutowapoteza marafiki zako, na kama kuna yeyote aliye rafiki atasumbuliwa na hili basi usihofu, kubali tu kumpoteza kwa kuwa hakuwa wa muhimu au wa msaada sana kwako.

Hali ya kujifanya hujaumia au hujakwazika na wakati umekwazika na unalia ndani kwa ndani inaumiza na kufanya ujisikie vibaya sana. Inakufanya uzidishe mazingira ya msongo wa mawazo (stress) hasa pale unapojiwazia wewe mwenyewe zaidi ya kushughulika na wale waliokuudhi. Mtazamo wako jinsi unavyojiona wewe mwenyewe huathirika sana, na pia waweza kujisababishia tatizo hasa pale wale wenye tabia ngumu watakapo kugundua kuwa huwezi kusema chochote hata ukiumizwa na hii itawafanya wakugeuze mpira wa kuchezea.

Je, wewe ni kati ya wale wanaojiamini kusema chochote wanachokifikiri bila kujali matokeo yake?

Hebu fikiria jinsi unavyojisikia pale ambapo mtu au watu wengine wangefanya hivyo hivyo kwako. Je, unataka kuwasababishia wengine maumivu ya moyoni? Kusema chochote kinachoshuka toka kichwani mwako kupitia kinywani mwako bila kufikiri juu ya matokeo au athari zake kwa wale wanaokusiliza au waliokuzunguka kunaweza kukupotezea marafiki na kuishusha hadhi yako kwa urahisi sana.

Mara nyingi mtu wa jinsi hii huweza kujikuta akiwa pweke na anayepingana na ulimwengu (kila mtu anamchukia). Hii ni kati ya hisia za kuhuzunisha na kuumiza sana muda wote, lakini pia huumiza zaidi pale unapogundua kuwa ni maumivu uliyojitakia mwenyewe. Peke yako unajikuta umetengwa na mtego wa kihisia na kukuzamisha usipoweza kujikwamua tena.

Kunyonyana ulimi au kula mate Kunasababisha kuambukiza VVU?


Swali: 
Je kunyonyana ulimi au kula mate kunaweza kuambukiza VVU?

Jibu:
Njia ya mdomo inaweza kuchangia mtu kupata VVU kama mtu atakutana na mtu mwenye VVU mwenye vidonda au michubuko mdomoni nawe pia ukawa una michubuko au vidondamdomoni, ili kuweza kupata VVU kwa njia ya mate inabidi kulambamate lita 2 jambo ambalo ni gumu.

Saturday, November 24, 2018

Makosa wanayofanya wanawake katika mahusiano ya kimapenzi


Zipo sababu mbalimbali ambazo huchangia mahusiano mengi ya kimapenzi kufa, na miongoni mwa tabia hizo ni pamoja na zile tabia ambazo wanawake hao wamekuwa wakiziendekeza na miongoni mwa tabia hizo ni kama ifutavyo;
  1. Kauli mbaya kwa mmewe. Unakuta mwanamke anarepu mbele ya mme wake utafikiri kafingiwa mota mdomoni.
  2. Uchafu. Unakuta baadhi ya wanawake akioga usiku mpaka usiku mwingine. Ngua ya ngani ukiangalia utafikiri mafundi wapiga plasta ukuta.
  3. Kukataa kufanya tendo la ndoa wakisingizia wamechoka.
  4. Dharau.
  5. Kuwa na michepuko ya wanaume wa nje.
  6. Pesa. Wanawake wakipata pesa uona wanaume wao si lolote.
  7. Elimu . Mwanamke akisoma na kumzidi mmewe basi anaona hata tendo la ndoa kufanyika maamuzi ni yake mwenyewe. Upatikanaji wa elimu kwa mwanamke umesababisha mahudiano mengi kufa.
  8. Madaraka. Ukifanya utafiti mdogo tu utakuta wanawake walio wengi wenye madaraka hawapo kwenye ndoa.  Wanaona kupata madaraka basi na masuala ya kimapebzi hayana nafasi yena.

Kanuni sita (6) za kudumu katika mahusiano ya kimapenzi


Hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa in . Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

Zifuatazo ni baadhi tu ya njia mbalimbali za kufanya ukae na mpenzi wako kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mkafurahia mapenzi yenu popote pale mtakapokuwa na mtakapoishi.

1. Kuwa na muonekano chanya kwa mpenzi wako.
Ukiwa ni mtu wa kuangalia mabaya/kasoro sana kwa mpenzi wako kuliko mazuri yake hautakuja kukaa kwenye mahusiano kwa muda mrefu hata siku moja, utaendelea kubadilisha Wmwanaume/Wanawake kila siku na mwisho wa siku utajiona huna bahati kwenye mapenzi na wakati Unayeyaharibu mapenzi yako ni wewe Mwenyewe...kakuna asiye na kasoro (Ukiwemo Wewe Mwenyewe).

Kwa hiyo muonyeshe mpenzi wako mapenzi bora na umrekebishe pale anapokosea Bila Kuwa Na Lawama Mara Kwa Mara, Kuna Makosa Mengine Ni Hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa in return. Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

Zifuatazo ni baadhi tu ya njia mbalimbali za kufanya ukae na mpenzi wako kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mkafurahia mapenzi yenu popote pale mtakapokuwa na mtakapoishi.

1. Kuwa na muonekano chanya kwa mpenzi wako.
Ukiwa Ni Mtu Wa Kuangalia Mabaya/Kasoro Sana Kwa Mpenzi Wako Kuliko Mazuri Yake Hautakuja Kukaa Kwenye Relationship Kwa Muda Mrefu Hata Siku Moja...Utaendelea Kubadilisha Wanaume/Wanawake Kila Siku Na Mwisho Wa Siku Utajiona Huna Bahati Kwenye Mapenzi Na Wakati Unayeyaharibu Mapenzi Yako Ni Wewe Mwenyewe...Hakuna Asiye Na Kasoro (Ukiwemo Wewe Mwenyewe). Kwa Hiyo Muonyeshe Mpenzi Wako Mapenzi Bora Na Umrekebishe Pale Anapokosea Bila Kuwa Na Lawama Mara Kwa Mara, Kuna Makosa Mengine Ni Madogo Sana Na Unaweza Kuyarekebisha Kwa Kukaa Chini Na Mpenzi Wako Mkayamaliza Kwa Dakika 5 Tu Lakini Wengine Huwa Issue Kubwa Kwao Na Kusababisha Mwisho Mbaya.

2. Samehe na kusahau.
Unapomsamehe mpenzi wako kwa kosa lolote alilokosa basi hakikisha umemsamehe kiukweli na ujitahidi kusahau kosa alilotenda itasaidia uwe na amani ya moyo zaidi kuliko kumsamehe kwa usoni tu lakini moyoni ukawa na Donge bado, hii hupelekea kupunguza mapenzi kwa kiasi Fulani kwake na kujikosesha furaha ya mapenzi.Anapokosea siku nyingine usimkumbushe kosa lake la nyuma kwa sababu itamfanya ajione mwenye huzuni na ajione kuwa hakusamehewa.

3. Mpe nafasi na uhuru mpenzi wako.
Mnapokuwa kwenye mahusiano jitahidini kwa hali na mali kupeana nafasi/uhuru kwenye mambo mengi hasa yale ya kitaaluma zaidi na kimaisha.anapokwambia yupo kwenye kikao cha kikazi jaribu kumuelewa na umpe support ya kutosha kwenye kazi zake au biashara zake au hata masomo yake.usipende sana kulalamika pale anapochelewa kurudi kazini au kutoka kwenye biashara zake bali mpokee kwa upole na baada ya kupumzika ndipo muulize kwa upole na kimahaba zaidi kwanini siku hizi anachelewa sana kurudi au kwenye biashara zake au shuleni tofauti na zamani.

Hii itajenga zaidi kuliko kubomoa kwa kulalamika na kupayuka mbele yake na huku yeye akiwa hata hajapumzika na itamfanya siku nyingine aione nyumba chungu kitu ambacho si kizuri kwenu wote wawili.

4. Kuwa mbunifu katika mapenzi.
Napozungumzia ubunifu hapa nakuwa simaanishi kwenye upande mmoja tu wa kwenye yale mambo yetu ya chumbani, hapana. Hapa namaanisha ubunifu kwenye mambo mengi ndani na nje ya nyumba, jitahidi mara kwa mara kubuni vitu vipya vitakavyofanya azidi kukupenda na kukuona kama mpya kwake kila siku. Kama amezoea kupata zawadi za aina Fulani kutoka kwako basi jitahidi siku moja kumbadilishia zawadi kutegemea na unavyomfahamu mpenzi wako anapenda nini na nini. Hakuna anayemjua mpenzi wako zaidi kuliko wewe kwa hiyo lazima ujue ukifanya nini kwake na kwa wakati gani atafurahia na kujivunia kuwa nawe.

5. Mfanye mwenza wako ajivunie kuwa nawe kila wakati.
Hakikisha katika mapenzi yenu kila siku unamfanya mpenzi wako ajivunie kuwa nawe na hakikisha humfanyi ajute kwa kukuchagua wewe miongoni mwa wote aliowaona. Usijidanganye hata siku moja kuwa kwa kumpata tu na kwa yeye kukupenda basi hajaona mwingine wa kuweza kuwa naye. Wapo wengi sana anaoweza kuwa nao lakini amekuchagua wewe katika hao wote, kwa hiyo usimfanye aanze kuwafikiria wale wengine wanaomfuatilia kila siku na kumsumbua.Ukianza kumwacha aanze kuwafikiria wengine aidha kwa wewe kuwa unamkosesha amani ya mapenzi kila mara au kwa mengine mabaya ndani ya mapenzi basi ipo siku utaishia pabaya.

6. Msadie kwa khali na mali kila inapowezekana.
Kwenye mahusiano huwa kuna kupanda na kushuka miongoni mwa wapenzi na hasa kiuchumi na hata kisaikolojia. Hakuna kitu kizuri kwenye mapenzi kama mtu kupata tatizo na akasaidiwa na mpenzi wake katika hali ambayo hakuitegemea, namaanisha mpenzi wako akipata tatizo lolote hakikisha wewe ndo unakuwa wa kwanza kulifahamu na kulifanyia kazi.

Sio matatizo yote yanamalizwa kwa pesa so hata ushauri na kumpa mawazo chanya inasaidia sana na kumfanya awe na furaha kuwa nawe.Kama unampenda usione tabu kumsaidia kwa kuogopa kuonekana eti unahonga, huyo ni mpenzi wako kwa hiyo jiamini na umpe kile anachostahili kusaidiwa na mpenzi wake.

Yapo mambo mengi sana ambayo kama mkiyafanya kwenye mapenzi basi uhusiano wenu utakuwa wa kudumu na wenye furaha sana ingawa hapa nimezungumzia kwa uchache sana lakini nina imani itasaidia sana kwa wote walio kwenye mahusiano .

Mapenzi hayana ndumba au limbwata hata siku moja, unapoona wapenzi wengi wana furaha kwenye mapenzi yao ni kwa sababu wanavumiliana kwa mengi na kusameheana kwa mengi. Sana Na Unaweza Kuyarekebisha Kwa Kukaa Chini Na Mpenzi Wako Mkayamaliza Kwa Dakika 5 Tu Lakini Wengine Huwa Issue Kubwa Kwao Na Kusababisha Mwisho Mbaya.

Kufanya mapenzi mara kwa mara kunaboresha afya yako

Kufanya mapenzi ni mojawapo ya vitu vichache ambavyo watafiti wanasema vinamfanya mtu aburudike huku mwili wake ukifaidika kutokana na tendo hilo.

Utafiti umeonyesha kwamba kufanya tendo la ndoa mara kwa mara kunatibu mafua, kuepusha magonjwa ya moyo, kunazuia kansa na hata kuongeza urefu wa maisha.

Watafiti katika chuo kikuu cha Nottingham University nchini Uingereza wamegundua kwamba wanaume wenye umri zaidi ya miaka 50 wanaofanya tendo la ndoa mara kwa mara wana uwezekano mdogo sana wa kupata kansa ya kibofu.

Watafiti hao walikanusha madai kwamba kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 20 kwa mwezi kunaongeza uwezekano wa kupata matatizo ya moyo.

Madaktari wamekubaliana kwamba mapenzi ni kama shughuli zingine za kawaida na ni mazoezi bora kwa afya.

"Kwa kulinganisha na mazoezi, kufanya mapenzi ni sawa na kutembea zaidi ya kilomita moja au kupanda na kushuka ngazi za majengo mawili marefu" alisema Dr Graham Jackson wa hospitali ya St Thomas.

Utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Queens University cha Belfast umesema kwamba kufanya mapenzi zaidi ya mara tatu kwa wiki kunapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo.

Tendo la ndoa pia linasaidia kulinda mifupa. Dr Sarah Brewer alisema: “kiwango cha Testosterone kimeonekana kuongezeka wakati tendo la ndoa na baada ya tendo la ndoa".

Utafiti huo ulibainisha kwamba kwa wanaume na wanawake ili waweze kupata faida za tendo la ndoa inawabidi wafanye tendo hilo mara kwa mara.

"Itumie au ipoteze" ndiyo ushauri uliokuwa ukitolewa kwa wazee na wanasayansi toka nchini Finland.

Pamoja na faida za tendo la ndoa ,tendo hilo pia lina hasara zake kama vile kupata magonjwa ya zinaa iwapo kinga haitatumika.

Tangia kugunduliwa kwa viagra miaka 10 iliyopita idadi ya watu wenye umri zaidi ya miaka 45 walioambukizwa magonjwa ya zinaa imeongezeka maradufu.
Ni ngumu na kamwe siyo rahisi kumbadilisha mtu mwenye tabia ngumu awe rafiki. Badiliko hili lawezekana ikiwa mhusika (mwenye tabia ngumu) atadhamiria na kuwatayari kushughulika ili kubadilika.

Kwa hiyo kama ni ngumu au haiwezekani kumbadilisha basi jaribu kubadili mtazamo wako na jinsi unavyoishi naye au nao, kwasababu mara nyingi wewe ndiye unaye kwazika au kuumizwa wakati yeye (yule anayekuudhi) anafanikiwa na anaendelea na furaha yake tu.

Mawasiliano baina yetu na watu wengine yanajumuisha jinsi tunavyowafanyia wengine na jinsi wao wanavyotufanyia sisi (reaction and counter reaction). Kwa kubadili jinsi sisi tunavyowatendea wengine inaweza kubadili jinsi wao wanavyotutendea sisi. Hata kama ni kwa muda au kitambo kidogo tu. Hata kama hali hii haibadili hali kwa kudumu ila inaweza kurahisisha mazingira ya kuishi na mtu au watu wenye tabia ngumu.

Kila wakati lazima uwe na akili sana katika kuishi na watu wenye tabia ngumu, kama hutoweza kujizuia, na ukaanza kuwabwatukia basi itakuwa unaleta tatizo hasa pale ambapo mwenye tabia hii ngumu ni bosi wako. Je, utaropoka au kutukana kama ulivyozoea?
Hata kama mtu au watu wenyetabia hii wako ndani ya familia na yamkini ni wadogo kwako kiumri, bado kuropoka na kuwapayukia siyo suluhisho, hali hii yaweza kukugharimu.

Najua kila mmoja wetu anajinsi anavyofanya kwa mtu au watu wenye tabia ngumu. Wote hatuna namna moja, mmoja anaweza kuwa ni mkimya na mwenye ujasiri hata anapoudhiwa, mwingine hupayuka na kumjibu yule anaye muudhi, mwingine anaamua kulia tu anapoudhiwa, wako wanaozira na kuamua kutozungumza tena na aliyewaudhi, wapo ambao husambaza habari mbaya kuhusu huyo mwenye maudhi, wako ambao huamua kumwambia uso kwa uso jinsi walivyo kwazika, sijui staili yako ni ipi.

Ni rahisi sana kuumizwa au kuudhiwa na maneno au matendo ya mwingine, na mara mtu huyo anapojua kuwa unaumia yeye hupata nguvu, hii huwa ndiyo silaha yake muhimu pale mnapopambana.

Unachotakiwa kufanya ni kuwaachia wakati wote wao wawe washindi, kamwe usitafute kushindana nao, utaumia mwenyewe. Njia pekee ni kujitahidi kuwa mjanja na mwenye akili kuliko yeye na pia kuwa na ushawishi katika yale wanayotaka kuyatenda hata pasipo wao kugundua.
Je, unawajibu vipi watu hawa (How do you react?)
Ni jambo jema kuanza kujitazama jinsi unavyowatendea wengine na jinsi tunavyoshughulika na wale wanaotukwaza. Kumbuka kuwa jinsi unavyoikabili hali hiyo katika mazingira fulani inawezekana isiwe hivyo katika mazingira mengine.

Watu wenye tabia ngumu na zinazotatiza mara nyingi huweka mitego ya maneno au matendo na kwa kiasi kikubwa unaweza kunaswa na kuwaruhusu wakuchezee jinsi watakavyo, na kati ya vitu wanavyo vipenda na kuvitamani ni kukuona unalia na kuumia na kuchanganyikiwa. Kwahiyo fikiri kwanza kabla hujafanya chochote mbele yao.

Watu watabia hii mara zote huwachukulia na kuwatendea watu wote sawa kwa hiyo usifikiri kila alichosema au alichofanya kwako ni cha kibinafsi sana na alikikusudia kwako. Angeweza kufanya au kusema hivyo hivyo hata kwa mwingine aliye karibu naye wakati ule. Kwa kufahamu hili itakusaidia kupunguza maumivu yanayoletwa na hisia zako kwake.

Hembu jiulize ni jinsi gani umewahi kukabiliana na mtu au watu wa jinsi hii, na je ilikuwa ni kwa jinsi ya kuumiza au kuelemisha? Fahamu kwamba kujibu kwa kupayuka, kutukana au kubishana haisaidii, bali kunakushusha chini ya miguu ya yule aliye kusababishia maumivu hayo, na sasa atakuwa anafurahia na kukuona wewe mjinga.

Ni chaguo lako, la ni jinsi gani utakabiliana na mtu au watu wa aina hii, ingawa unaweza kuchagua njia bora itakayoweza kukusaidia kukuimarisha na kupunguza udhaifu wako, zaidi ya kuamua kuchagua njia ambayo itakuacha umeumia, umechoka, umekatishwa tamaa na umejeruhika moyo.

Hii haimaanishi uwe mtu wa kusema ndiyo tu kwa kila kitu na kila mtu, na haimaanishi kuwa hutakiwi kukasirika HAPANA, hasira ni asili na haina tatizo lolote hapa, ila tu matokeo ya hasira hiyo ndiyo yanayoweza kuleta shida. Je ni jinsi gani unakabiliana na hasira yako na unaionyeshaje? Kwa fujo, kupayuka kubishana, kulia, kuvunja vitu, kunyamaza n.k.

Ili Kujua jinsi watu wenye tabia ngumu wanavyokuathiri. Jiulize maswali yafuatayo:
Je, ni unataka kutawaliwa na wengine?
Najua jibu ni kwamba hakuna nayetaka kutawaliwa na mwingine, na ndiyo maana unaweza kujikuta unabishana au kushindana na huyo anaye kukwaza.

Tatizo ni kwamba mwisho wewe ndiyo unaumia na yeye anabaki kufurahia kwa kukushinda mfano; tazama fujo za madereva barabarani hususan wale wa daladala.
Nikweli unahasira naye, lakini je hiyo ni njia muafaka ya kumkabili? kumbuka mwishoni atakayeumia ni wewe.

Fikiri kama unatatizo la shinikizo la damu kama utakubali kuyumbishwa kihisia na tabia mbovu za mwingine wewe ndiyo utabaki unaumia na siyo tu kama hutoweza kufanya vile moyo wako utakavyo bali pia utaachwa ukijihisi kuchoka, kuumizwa kwa hisia zako mwenyewe na kukatishwa tamaa na tabia yako wewe mwenyewe.

Nini Mwitikio wako pale unapoudhiwa? (Haswa na yule mwenye hasira na wewe)
Je, unalipa hasira kwa hasira?
Je, unajitetea na kuukimbia ukweli (being defensive)
Au unajificha kutoroka au kumkwepa?
Njia zote hizi hapa juu siyo nzuri.

Hata kama una haki ya kukasirika, lakini bado atakayeumia unabaki kuwa ni wewe. Na siyo tu utaumizwa na kukasirishwa kwa tabia yake mwenye kukuudhi bali utaumizwa moyoni mwako kwa vile wewe ulivyotenda, dhamiri itakushtaki zaidi (guilty conscious).

Je, unajizumgumziaje wewe mwenyewe, vibaya au vyema?
Mfano: Ukweli mimi najichukia haswa ninapofikia kipindi cha mitihani au usaili.
Hivi mimi nikoje?
Hivi kwa nini nimeumbwa hivi?
Kamwe mimi siwezi kufanya lolote jema!
Wakati wote mimi ni mtu wa bahati mbaya tu!

Wala huhitaji kujichukia unapofikia wakati wa mitihani au usaili, unachohitaji kufanya ni kujiandaa mwenyewe vizuri na kuwahi mapema katika eneo la tukio.
Hisia potofu na zisizojenga ambazo tunajiwazia wenyewe mara nyingi hutupotezea muda na mara tunapoziruhusu hutuharibia siku yetu nzima.

Unafanya nini unapopingwa? (what do you do when you are criticized)
Wako watu wanaopendelea kupinga wengine katika kila kitu, hata katika vile visivyostahili kupingwa,hakuna chochote chema kinachoweza kusemwa na yeyote, bali yeye peke yake. Hata kama kilichosemwa kina ukweli kwa asilimia kubwa basi mtu huyu atajitahidi walau kurekebisha hata lugha tu, ili mradi kisipite hivihivi bila yeye kukipinga japo kidogo (hawa ndiyo wale wenye tabia ngumu).

Hali hii huwapa kufurahi na kujijengea nguvu kwa jinsi wanavyopinga wengine.
Ni kweli upinzani mwingine ni wa ukweli na unajenga lakini hapa nakazia wale wanaopinga ili tu kujifurahisha nafsi zao na kuwafanya wale wanaowapinga waumie mioyo.

Je, unapopigwa, unajibuje? Je, unajitetea au unajishusha na kukubali kila kinachopingwa kwa kuamini kwamba anayekupinga yuko sawa na kwa hiyo unayameza maoni yako yote, bila kuchambua kwa kina mapingamizi hayo.

Kuna jinsi ambavyo unaweza kumkabili au kumjibu anayekupinga na ikawa kama umeweka petroli kwenye moto, upinzani utawaka na hata kuleta ugomvi, lakini pia iko njia ambayo unaweza kumjibu mtu huyu na ukanyamazisha fukuto lote.

Je, una mtazamo hasi (mtazamo usiofaa) na wa kudumu katika kitu fulani?
Mfano; Labda unasema “Mambo yangu hayaendelei tangu nihamie katika nyumba hii, au mambo yangu yanakwama tangu nimuoe au niolewe na huyu, ni matatizo tu tangu tuoane, watoto hawa hasara tupu.” n.k.

Mtazamo huu hasi, waweza kukugharimu siyo tu kukunyima raha bali pia waweza kuharibu hisia zako na za wengine pia.
Ukijikuta katika hali hii ni vyema kujifahamu na kujitahidi kuelewa nini tatizo husika na jitahidi kubadilisha mtazamo wako.

Tafuta vile vitu ambavyo unaweza kuvitazama katika mtazamo chanya hata kama ni vidogo. Tafuta kuviongelea vile unavyovipenda zaidi ya vile usivyovipenda.
Je, unazimeza hisia zako zote, nzuri na mbaya?

Je, unaona ni ngumu sana kusema “nakupenda” “umependeza” “umeniudhi” n.k. labda unaweza kusema neno moja tu na siyo lingine. Wengi wetu tumekuzwa katika mazingira ambayo tunahofu kusema chochote ili tu tusije tukamkwaza mtu, hata kama tunaumizwa au tunajisikia vyema kusema kitu fulani, lakini tunajizuia.

Badala yake tunakwenda kusemea pembeni. Yamkini kunyamaza kunaweza kuwa na faida katika baadhi ya mazingira lakini siyo hata katika kukubali vitu visivyofaa. Hakuna ubaya wowote katika kuelezea jinsi unavyojisikia moyoni mwako ili mradi tu unaeleza kila unachokihisi kwa hali njema na siyo kwa hasira au shari. Katika hali hii kamwe hutowapoteza marafiki zako, na kama kuna yeyote aliye rafiki atasumbuliwa na hili basi usihofu, kubali tu kumpoteza kwa kuwa hakuwa wa muhimu au wa msaada sana kwako.

Hali ya kujifanya hujaumia au hujakwazika na wakati umekwazika na unalia ndani kwa ndani inaumiza na kufanya ujisikie vibaya sana. Inakufanya uzidishe mazingira ya msongo wa mawazo (stress) hasa pale unapojiwazia wewe mwenyewe zaidi ya kushughulika na wale waliokuudhi. Mtazamo wako jinsi unavyojiona wewe mwenyewe huathirika sana, na pia waweza kujisababishia tatizo hasa pale wale wenye tabia ngumu watakapo kugundua kuwa huwezi kusema chochote hata ukiumizwa na hii itawafanya wakugeuze mpira wa kuchezea.

Je, wewe ni kati ya wale wanaojiamini kusema chochote wanachokifikiri bila kujali matokeo yake?

Hebu fikiria jinsi unavyojisikia pale ambapo mtu au watu wengine wangefanya hivyo hivyo kwako. Je, unataka kuwasababishia wengine maumivu ya moyoni? Kusema chochote kinachoshuka toka kichwani mwako kupitia kinywani mwako bila kufikiri juu ya matokeo au athari zake kwa wale wanaokusiliza au waliokuzunguka kunaweza kukupotezea marafiki na kuishusha hadhi yako kwa urahisi sana.

Mara nyingi mtu wa jinsi hii huweza kujikuta akiwa pweke na anayepingana na ulimwengu (kila mtu anamchukia). Hii ni kati ya hisia za kuhuzunisha na kuumiza sana muda wote, lakini pia huumiza zaidi pale unapogundua kuwa ni maumivu uliyojitakia mwenyewe. Peke yako unajikuta umetengwa na mtego wa kihisia na kukuzamisha usipoweza kujikwamua tena.

Kukumbatiwa na umpendaye wakati wa maumivu kuna nguvu zaidi ya dawa Paracetamol


Kumbatio kutoka kwa mtu umpendaye, linaweza kuwa na nguvu zaidi ya Paracetamol pale unapokuwa na maumivu, kwa mujibu wa utafiti.

Wanasayansi wamebaini kuwa hisia za ukaribu tunazozipata kupitia mtu anayetushika, kunaweza kusaidia kupunguza maumivu. Lakini kushikwa na mtu usiyemjua, kunaweza kusiwe na matokeo yale yake, kwasababu hatuna hisia nao.

Utafiti huo unaonesha nguvu ya ubongo kuzuia hisia za maumivu. Utafiti huo ulifanywa na wataalam katika chuo kikuu cha Haifa, Israel na ulihusisha wanawake kadhaa ambao waliwatengenezea maumivu kwa kuwaunguza na chuma chenye moto kiasi.

Katika jaribio la kwanza, mtu wasiyemjua aliwashika mkono akijaribu kuwaliwaza kwa maumivu hayo. Kwenye la pili waliwaita waume na wapenzi wao kukaa karibu nao na kugusanisha ngozi.

Katika jaribio la mwisho, wapenzi wao waliruhusiwa kuwashika mkono wakati chuma hicho cha moto kikigusishwa kwenye ngozi zao. Wanasayansi walibaini kuwa mguso wa mtu wasiyemjua pamoja na kuwa na mpendwa wao karibu hakukuwa na tofauti katika jinsi walivyosikia maumivu.

Lakini pale mtu wanayempenda alipowagusa kwenye ngozi, maumivu yalipungua.
Walibaini pia kuwa kadri mpenzi wa mwanamke alivyoonesha huruma na support kwake wakati wa zoezi hilo, alipata afueni zaidi.

Kabla ya kufunga ndoa hakikisha mmepima haya magonjwa 4 ya kuambukizwa


1. Ugonjwa wa kaswende.
Kitaalamu kama syphilis, huu ni ugonjwa hatari sana ambao umeharibu maisha ya watu wengi bila wao kujifahamu. Ugonjwa huu ambao huambukizwa kwa njia ya kujamiana huanza kidogo na kidonda ambacho hakiumi sehemu ambapo wadudu wamepita mfano mdomoni au sehemu za siri.

Kidonda hicho hupona, upele usiowasha hutokea na baadae vyote hivyo hupotea. Ugonjwa huu baadae huingia ndani ya mwili na kuuanza kuharibu viungo vya ndani. Mwisho kabisa ugonjwa huu huahamia kwenye ubongo na kumfanya mtu kua kichaa.

2. Ugonjwa wa hepatitis B.
Ugonjwa huu ni hatari na unaua haraka kuliko ukimwi, virusi vya ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya kujamiana na kugusana kwa damu au majimaji ya mwili kama ukimwi lakini ni rahisi zaidi kuambukizwa ugonjwa huu kuliko kupata ukimwi.

Ugonjwa huu hushambulia maini na kuacha makovu, Mgonjwa hupata macho ya njano, homa, maumivu ya kichwa na kadhalika. Ugonjwa hii mwishoni hupelekea kansa ya ini ambayo inaua ndani ya miezi sita.

3. Ugonjwa wa ukimwi.
Huu ni ugonjwa unaofahamika kwani unatangazwa sana hasa kwenye vituo vya Radio, Tv, Magazeti na sehemu mbalimbali.

Ugonjwa huu uligundulika karne ya 20 na mpaka sasa umeshaua watu wengi sana na zaidi ya 95% ya wagonjwa waliambukizwa kwa kushiriki ngono bila kinga.

4. Ugonjwa wa gonorea.
Huu ni ugonjwa wa zinaa ambao unashambulia jinsia zote yaani Wanaume na Wanawake, mara nyingi Mwanaume hawezi kujificha na ugonjwa huu kwani dalili za ugonjwa huo kama kutoka na usaa kwenye njia ya kukojolea zitamuumbua lakini kwa wananwake ugonjwa huu huweza kukaa kimya na mwana mke hujikuta akisambaza ugonjwa huo bila kujua. Mwishoni ugonjwa huu hushambulia kizazi na kusababisha ugumba.

Bill Nas Ajitapa Kuwa Hajawahi Kuachwa na Mwanamke

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Bill Nas ameibuka na kudai kuwa kwenye maisha yake yote hajawahi kuachwa na mwanamke kwenye mapenzi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari katika siku za Hivi karibuni Billnass amesema kuwa amedate na watu wengi sana huku akisema neno wengi linaanzia na mbili lakini hajawahi kuachwa.

Mimi sijawahi kuachwa kwenye mahusiano kama kuna dada ana prove amewahi kuniacha na nimedate na watu wengi kidogo sio wengi sana kwasababu wengi inaanzia na mbili sasa sikujua anamzungumzia dada gani lakini kwa bahati sijawahi kuachwa nikiona vitu haviendi naamua kufanya vitu vingine“.

Billnas alitengeneza headlines miezi michache iliyopita Baada ya video yake ya faragha na Mpenzi Wake Nandy kusambaa katika mitandao ya kijamii.

Ijue misingi ya Uvumilivu katika Ndoa


Ni wazi kuwa migogoro kwenye uhusiano wowote ule ipo, hasa pale wenza hao wasipopeana nafasi ya kusikilizana.

Kila siku narejea hii hoja kuwa, hata kwenye uhusiano wa mapenzi lazima kutakuwepo na mikwaruzano ya hapa na pale jambo la msingi ni namna ya kushughulikia misuguano hiyo bila kuibua chuki na hatimaye kuvunja uhusiano.

Hata katika uhusiano wa kawaida, mikwaruzano na misuguano ni kama kukanyaga bomu, bila kuchukua tahadhari na kutegua bomu lenyewe, ukiondoa mguu mtu bomu hilo linalipuka na kuharibu kila kitu.

Uvumilivu ndio jibu kubwa kwa wenza endapo itatokea kukwaruzana au kutoelewana.
Endapo mwenza wako amekuudhi na kukupandisha hasira jambo la msingi kabisa ni kuhakikisha unadhibiti hasira hizo. Jaribu kuelewa kwanza tatizo kabla hasira hazijakuathiri na kukutawala.

Kumbuka kuwa hasira hasara na siku zote mtu mwenye hasira huzungumza na kufanya mambo ambayo baadaye hujikuta akijilaumu. Lakini pia watalamu wa masula ya mahusiano wanasema ya kwamba siku zote epuka kuchukua maamuzi ukiwa na hasira.

Unapotokea msuguano katika mapenzi epuka kuwa mzungumzaji na mlalamishi, kuwa mtulivu na tanguliza busara mbele kabla ya kutamka chochote kinywani kwako.

Huo ndio msingi wa uvumilivu.
Katika hili, vitabu vingi vya uhusiano vinashauri kuwa endapo mwenza anaona hali na mazingira ya mazungumzo hairidhishi kutokana na ugomvi wenyewe ni bora kuahirisha mazungumzo hayo na kupanga muda mwingine wakati wote wawili wakiwa wametulia.