
Msichana ana miaka 22, anafuatwa na mvulana na kuambiwa kwamba anataka
kuolewa, mvulana yupo kamili, kajiandaa na anamaanisha, msichana
anakataa kwa visingizio vya kipimbavu, mvulana anaachana nae.
Anachokifanya ni kumfuata mtu ambaye hana mpango wa kumuoa, kisa gari
kisa fedha anataka kuitwa mpenzi na mambo kuishia kitandani.
Haiishii hapo, anapofika miaka 23, 24, 25, 26 hali inakuwa hivyo hivyo,
kwake, anajiona hana haja ya kuolewa, anaamua kuwa na mpenzi tu, leo
huyu, kesho huyu na keshokutwa yule.
Siku hazimsubiri, miaka 27, 28, 29 na 30 inaingia, hapo ndipo anashtuka
kwamba kapoteza muda na anatakiwa kuolewa. Hahaha! Mungu sio chizi.
Mungu aliyajua maisha yako ya mbele, akakuletea wanaume mbalimbali wa
kutaka kukuoa lakini ukakataa kwa sababu zisizo na mantiki. Kuolewa
hauolewi, unaanza kuhangaika huku na kule, kila mwanamme kwako
anaonekana kuwa muhimu. Yaani wakati ambao hukuuhitaji ndoa, ndoa
ilikuhitaji na wakati ambao unaihitaji ndoa, ndoa haikuhitaji.
Kwa mahesabu, kama una miaka 30 inakupasa kuolewa na mwanaume mwenye
angalau miaka 33 au 35. Je kuna mwanaume mwenye umri huo ambaye yupo
tayari kuoa? Mwanaume hataki kuitwa babu na mtoto wake, anataka kuitwa
baba. Mwanaume anapofikisha umri wa miaka 30 anaweka jiko ndani lenye
miaka chini ya 25. Sasa katika kipindi alichokuwa na miaka 30,
ukamkataa, wewe ukiwa na miaka 30 mwenzako ana 35, keshaoa kitambo.
Sikulazimishi uolewe ila unapopata mwanaume aliye radhi kukuoa, kubali
tu, ndoa ni bahati, kuna wanawake wanafikisha miaka 40 na bado
hawajaolewa na kila siku wanatamani kuolewa. Unapoipata bahati, fanya
mambo. Siku zote mwanamme anapokwambia kwamba anataka kukuoa, ukaleta
pozi weeeeee, akija kwa mara ya pili, huyo si muoaji, atakuja,
atakuchezea na kukuacha, alikupa nafasi ukailetea pozi.
WANAWAKE WAPO MILIONI 29 TANZANIA NA WANAUME MILIONI 25. HALAFU WEWE UNALETA POZI...HAYA, NGOJA TUONE MWISHO WAKE.
Hii ni kweli kabisa, Kwa Dada zangu kuweni makini maana daima muda hauna subira
ReplyDelete