Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Saturday, June 30, 2018

Wapenzi Watiwa Mbaroni kwa Kufanya Mapenzi Kabla ya Ndoa...!!!!

RAIA mmoja wa Afrika Kusini na mchumba wake kutoka nchini Ukraine wametiwa mbaroni nchini Falme za Kiarabu kwa kufanya mapenzi kabla ya ndoa, ndugu amebainisha.
Emlyn Culverwell, 29, na Iryna Nohai, 27, waliripotiwa kukamatwa baada ya daktari kugundua kwamba Nohai, ambaye alikuwa na maumivu ya tumbo, alikuwa na ujauzito.
Walikamatwa kwa kufanya mapenzi nje ya ndoa, jambo ambalo ni kinyume cha sheria nchini humo.
Mama wa Culverwell ameomba waachiwe huru, kwa kusema “kitu pekee walichofanya kibaya ni kupendana.”
Wizara ya mambo ya nje ya Afrika Kusini ilisema kwamba haitoweza kuwasaidia wapenzi hao kwa kuwa ni suala la ndani la sheria za Falme za Kiarabu, mtandao wa News24 uliripoti.
Serikali ya Afrika Kusini imewashauri wapenzi hao kutafuta msaada wa kisehria, mwandishi wa BBC huko Johannesburg anasema.
Hadi sasa hakuna maelezo yoyote kutoka serikali ya Falme za Kiarabu.
Culverwell na Nohai wanaripotiwa kuwa wanashikiliwa tangu mwezi Januari mwaka huu, lakini taarifa juu ya kushikiliwa kwao zimeanza kujulikana sasa.
Culverwell amekuwa anafanya kazi nchini Falme za Kiarabu kwa miaka mitano sasa.
Mama yake Linda aliuambia mtandao wa News24 kwamba familia yake inajaribu “kupeleka ujumbe kwa wawili hao na kuwaambia kuwa inawapenda na kwamba hawapaswi kuwa na wasiwasi.”
Wapenzi hao bado hawajafunguliwa mashtaka kwa kuwa mamlaka nchini humo bado wanawafanyia uchunguzi wa kiafya.
Iwapo watakutwa na hatia, wanaweza kukabiliwa na kifungo cha muda mrefu.
FacebookTwitterGoogle+WhatsAppPinterestShare

1 comment:

  1. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159

    ReplyDelete