Kumtafuta mwandani wa moyo wako kwenye mtandao ni jambo la kuvutia sana;
japokuwa kuna umuhimu wa kupata hatari. Kwasababu tayari una aina
nyingi ya watu, lakini pia huna uzoefu wa kukutana na jamii kubwa ya
watu na unawakati mgumu kupambanua ni mtu yupi anakidhi vigezo vya mtu
unayemtafuta. Sasa yapo mambo ya kuzingatia katika matazamio yako ya
kumtafuta mchumba wako ndani ya mtandao. Hivi vitu adimu ambavyo naenda
kukupa vitakusaidia kukuweka mbali na mwanaume au mwanamke ambaye siye
unaye mtafuta.
Jambo la 1.
Anza taratibu. TAMBUA HII kuwa kuna aina ya yote ya watu katika
himaya ya mapenzi; na siyo watu hawa wote watakufaa. Chukua muda wako
–kama umekutana na mtu kwa mara ya kwanza na anza mazungumuzo ama
kuchati naye taratibu na kumgundua kama ndiye. Mtu huweza kujisifu kuwa
yeye yuko hivi ni mpaka wewe umgundue hivyo na sisitiza kuwa chukua
muda wako kumchunguza kwa makini tabia yake ya mwazo na ya sasa. KAMA
KUNA KITU kimekutatiza ni RAHISI TU achana naye. Chukua virago vyako.
KAMWE USIKIMBILIE MAHUSIANO YOYOTE YA KIMAPENZI KABLA YA KUFIKIRIA
KWANZA.
Jambo la 2.
Linda Utambulisho wako (protect your Identity). Moja ya faida ya
kumatafuta umpendaye kwenye matandao ni kwamba utajikuta unamjua mtu
haswa kulingana na haiba yake. Inabaki kuwa uamuzi wako kuwa ni wakati
gani kujionyesha kuwa wewe ni nani haswa lakini yakupasa kuwa makini
sana, Ingawa pale mtu anapopokea haiba (personality) anaweza kuitumia
kinyume na matwakwa yako. Kama mwenzako anakupa presha juu ya wewe
kumpa jina lako la mwisho, email yako, anwani ya nyumbani kwako, namba
ya simu, na mahala ambapo unafanyia kazi na vitu
vinginevinavyokutambulisha wewe…ACHANA NA HUYO MTU.
Jambo la 3.
Tumia Akili. Wakati unapozungumza na mtu kupitia himaya ya
Mapenzi, usitupe maamuzi mazuri mbali eti kisa hii ni huduma ya
kimtandao. Jambo ambalo linaweza sikika vizuri na likahamasisha ni kuwa
umempata mtu ambaye umemjua vizuri. Kuwa na tahadhari na uzitumie hizo
tahadhari, na USIANGUKE katika kumpenda mtu eti kwasababu umevutiwa na
wasifu wake uliousoma kwenye mtandao. Chukua muda wako pia pitia kila
maeneo muhimu.ya chaguo zako. Baada ya kufanya utafiti wa kutosha na
kujiridhisha vya kutosha. Ni mazoea sana watu huanguka katika mapenzi
baada ya mazunguzo ya kwanza. USIRUHUSU HILI. Jitahidi kudumisha akili
yako na kuona kuwa kumtafuta umpendaye kwenye mtandao ni sawa na
utafutaji wa mchumba ndani ya dunia yetu hii ya kawaida. Haipaswi
kupenda kila wasifu unaousoma.
Jambo la 4.
Omba Picha. Unapokutana na mtu, chati naye, na ona jinsi mwanzo
wa mahusiano unavyokuwa unajengwa hapo itakupeleka kuona kuwa unaweza
ukaomba picha. Hii itakupelekea hasa kukupa taarifa zaidi kuhusu mtu
mwenyewe kuliko email na chating zingine zinazofanyika. Awali ya yote
itaondoa uongo wa kila mtu anavyomtazamia mwenziye kuwa yukoje. Utajua
pia anakuvutia kimuonekano? Ama La! Mwisho kama anashindwa kutuma picha
yake, huenda kukawa na sababu. NENDA KWA UANGALIFU
Jambo la 5.
Kuwa Makini. Hili linawezekana, ni jambo la muhimu sana
ukilifuata. Katika email, kila mtu anaweza kusikika vizuri lakini katika
uhalisia si yeye .mnapokuwa umejiingiza katika himaya ya uchumba ama
mapenzi na mtu pia tegemea bendera nyekundu ama tabia za zamani. Pia
weka umakini katika majaribio yoyote ya kukupa presha ama kukutawala.
Mwisho angalia sana na kuwa makini na taarifa zile ambazo mchumba wako
anakupatia ama majibu ya maswali unayomuuliza. Kama uhusiano wako
unaonyesha mambo yafuatayo. Unashauriwa kuangalia upya mahusiano yako;
1. Kama mwanamke/ mwanaume hatoi majibu ya kweli kuhusu umri wake, vitu anavyopendelea, mwonekano, taaluma yake na ajira yake.
2. Kama anakataa kuongea na wewe kwenye simu baada ya kuanzisha mahusiano ya kwenye mtandao.
3. Kama hatoweza kujibu kwa ufasaha maswali mtakayokuwa mnaulizana. Je
atakuwa anakujibu maswali vizuri ama anakurudishia swali kwako.
4. Kama atakupa picha ya kikundi cha watu waliyopiga pamoja na yeye
akiwemo itakayofanya kuwa vigumu kumtafuta.
Kutafuta mchumba mzuri umpendaye kwenye mtandao ni jambo zuri na
linahamasisha na linatimiza ndoto zako. Wewe kumbuka tu kufuata mambo
muhimu hapo juu na fanya kama yanavyoelekeza na utafanikiwa.
No comments:
Post a Comment