Mchungaji Peter Mitimingi akiwa na mkewe Patience
Ndoa katika jamii za kikristo zilikusudiwa kudumu na kuwa mfano wa
kuigwa na ndoa za watu wengine katika jamii. Lakini cha kushangaza ndoa
nyingi leo za kikristo zinavunjika kwa kasi ya
kushtusha. Hii inashtusha na kushangaza kwa sababu sisi kama wakristo
tumeacha kutembea katika mpango kamili wa Mungu. Kwanini hali hii
inatokea? Kuna sababu nyingi kwanini ndoa zinakuwa na migogoro isiyoisha
na ningine kutawanyika. Kuna sababu ndogo ndogo na zingine ni kubwa na
za msingi.
Zifuatazo ni baadhi ya Sababu Kwanini Ndoa nyingi siku za leo zimejaa Migogoro, Marumbano na Kuvunjika vunjika.
USIOE AU KUOLEWA KWASABABU YA KUMSAIDIA MTU FULANI AU KUMUONEA HURUMA
1. Kuoa au Kuolewa na Mtu kwasababu ya Kumuonea Huruma.
• Kuoa au kuolewa na mtu kwa sababu ya kumuonea huruma ni moja kati ya
sababu zisizo sahihi. Na inaonekana kuwa ni sababu moja ya kijinga pia.
•Ndoa zianazo oana kwa misingi ya kumsaidia mtu au kumwonea mtu huruma
huwa hazina maisha. 2. Huruma ya Kujiona kuwa ni wewe Ndio Unawajibika.
Kumhurumia mtu na kujiona kuwa una wajibu wa kumsaidia ni vizuri, lakini
kuolewa naye kwa sababu hiyo ni wazi kuwa ni jambo lisilo la hekima
kabisa.
3. Ndoa niyathamani Kuliko Huruma ya Mahusiano.
• Ndoa ni kitu cha thamani zaidi kuliko mahusiano ambayo yamejijenga katika huruma.
Chukulia kwamba kama mhusika ana masaa sita tu kuishi baada ya ndoa. Kwa
hiyo utaishi katika ujinga huo kwa masaa sita tu maana kinyume na hapo
utaishi maisha yako yote ukiwa unajihisi mjinga zaidi na mwenye huzuni.
• Hiyo itakuwa ni sabau ya kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa sababu utaonekana mbaya zaidi ya kabla hujaingia.
4. Kuoa au Kuolewa kwajili ya Kumsaidia Mtu Anayeteseka.
•Usioe au kuolewa na mtu eti kwasababu unaamua kumsaidia kutokana na shida Fulani.
• Mfano kuna baadhi ya watu utakuta mwanaume anaamua kumuoa msichana
fulani eti kwasababu kule anakoishi wanamnyanyasa na kumtesa so anaamua
amsaidie amuoe ili aishi naye.
• Hii ni sawa na ile ya ujinga wa kufikiri kwamba utaoa au kuolewa na
mtu kwa matumaini kwamba utambadilisha mtu baada ya kuolewa au kumuoa
ili afanane na wewe, dini yako au tamaduni zako.
• Kumbuka kwamba, kuwa na jitihada za kukubaliana sio kubadilika, sababu
suala ndoa halina haja ya kuweka mabadiliko kwa mtu yeyote.
• Ukitaka kumbadilisha mwenzi wako usisubiri kwenda kumbadilishia ndani fanya hayo mabadiliko kabla ya kuingia ndani.
No comments:
Post a Comment