Makamu
wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu amewahasa wanaume wote wa
Tanzania kutowaona wakubwa wenzao wamechuja katika tendo la ndoa na
kuanza kuwataka watoto wadogo ambao ni watoto wao na taifa la kesho.
Akizungumza
leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam wakati wa
maadhimisho ya siku ya Ukimwi ambapo pamoja na hilo amesema wapo baadhi
ya wanaume ambao wanajua wameshaambukizwa bado wanaendelea kuwaambukiza
watoto hao.
“Wanaume
msipende kuwaona wakubwa wenzenu wamechuja hawana ladha ile ambayo
mngependa kuipata, kwahiyo mna hamia kwa watoto wadogo ndugu zangu huu
sio mwendo mzuri hawa ni watoto wetu, hili ni taifa la kesho
tukiliteketeza leo, na wengine wanajua wameshaambukizwa na wakubwa
wanaushifti kwa watoto wadogo ambao ambao hawawajui, ndugu zangu huu ni
uuwaji wa makusudi na Mwenyezi Mungu hatawasamehe katika hili,” amesema Mama Samia.
No comments:
Post a Comment