Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Thursday, October 18, 2018

Msichana ni Mzurii Lakini Haeleweki..Naombeni Ushauri




Kuna msichana ambaye ni Jirani yangu sana na kusema kweli ni mzuri sana. Nilipataga hofu ya kumtongoza kwa sababu ya uzuri wake na ni gate kali. Ila kila alipokuwa anapata upenyo anakuja getto kwangu tunacheki movies na kula kwangu.


Siku moja nikajisemea moyoni kuwa Jamii na masela wangu wataniona kama sitampa mtoto haki yake mbali na kumuoa. Basi kidume nikajipanga na alivyo kuja kwa mara ingine gheto nikampa makavu live bila kupepesa macho. msichana aliniangalia na hakuweza kusema kitu akang'oa nanga na kuondoka.

Sikuwa na haja ya kumsihi arudi kwani alikasirika,ila moyoni nilijua massege sent. Ikapita kama wiki mbili bila kumwona tena ila kwa bahati nilikuwa nakatiza mtaani nikakutana nae akitokea sokoni nikampa hi na akaipokea bila kusita.

Nilivyompita na kumwacha nyuma aliniita "Ras" Lete habari,naomba unisaidie haka kamfuko huku akinitazama kwa jicho la madaha akiashiria kukubalian na ile sms nliyomtumia.

Basi tukiwatunasonga na safari huku story za hapa na pale nikaona ni vyema kumuuliza vp juu ya ile sms. Cha ajabu alikasirika zaidi ya mwanzon na kuninyang'anya kale ka mfuko na kuniambia nimemboa na hataki kampan yangu wala swaga zangu.

Naommbeni ushauri wenu nimfanyie Suprise gani huyu msichana ili anielewe kuwa nampenda.

No comments:

Post a Comment