Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Saturday, October 20, 2018

Mwanamke Kumkimbia Mume Maisha yakiwa Magumu na Kurudi yanapokuwa Mazuri.



Nimeleta mada hii tujadili tuone ni wapi mtu anapokuwa sahihi na wapi mtu anakosea.

Mkataba wa ndoa unawataka wanandoa kuvumiliana katika SHIDA na RAHA.

Sasa chukulia mmeoana halafu inafikia mahali maisha yanakuwa magumu hata milo miwili inashindikana, hivyo mwanamke anaamua kumkimbia mumewe.

Mwanaume anapobaki mwenyewe anaparangana japo maisha yanarudi kwenye mstari, na hapo mwanamke anaanza kutaka kurudi tena kwa nguvu kwakuwa bado ni mke halali.

Usahihi wa huyu mwanamke ni upi. Kabla hajaingia kwa nyumba, mwanaume alikuwa vizuri na pengine mwanamke alichangia ufukara katika familia hiyo kwani alipoondoka, mali zilirejea, na yeye akataka kurejea tena. Je kama wewe ndo mwanaume utampokea tena? Tuangalie pande zote.

Karibu tuchangie.

No comments:

Post a Comment