UTAFITI umebaini kuwa wananchi wa Rwanda wataendelea kuongoza katika
kuishi miaka mingi katika nchi za Afrika Mashariki mpaka 2040 na
kufuatiwa na wananchi wa Kenya.
Mabadiliko hayo yanatokana na aina ya vyakula na mazingira wanayoishi.
Kwa sasa Rwanda ina wastani wa uwezo wa kuishi akiwa miaka 67.8, ikikua
kufikia miaka 74.8 na hali ikiendelea vema itafikia miaka 77.6 kwa
mazingira bora ya afya.
Kenya ikishika nafasi ya pili katika nchi za ukanda huo ikiwa na wastani
wa wananchi wake kuishi miaka 66.9 huku ikitarajiwa mwaka 2040
itaongezeka kwa miaka 73.9 na ikiwa serikali itaboresha huduma za afya
itakua kwa miaka 78, hivyo kuchukua nafasi ya Rwanda.
Akitangaza jijini Washington, Marekani juu ya utafiti mpya uliochapishwa
na gazeti la Tiba la Kimataifa la The Lancet, Mkurugenzi wa Takwimu
katika Taasisi ya Afya na tafiti, Dk Kyle Foreman, alisema Tanzania
wastani wa umri wa kuishi kwa sasa ni miaka 64.3 huku ikitarajiwa
kufikia miaka 72.3 kwa mikakati ya sasa na ikiboreshwa zaidi itafikia
miaka 75.9.
Kwa sasa Uganda ina wastani wa umri wa kuishi wa miaka 62.2 na
ikitarajiwa kuongezeka kufikia umri wa miaka 69.5 mwaka 2040, huku mwaka
2040 ikitarajiwa kuongezeka mpaka miaka 72.8 ikiwa huduma za afya
zitaboreshwa.
Utafiti umeonesha kuwa changamoto kubwa ya umri wa kuishi ni magonjwa
yasiyoambukizwa yanayotarajiwa kuwa sababu kubwa ya vifo vya watu katika
nchi za Afrika Mashariki ifikapo 2040, yakiwemo kisukari, figo,
saratani za aina mbalimbali na uzito uliokithiri.
Friday, October 26, 2018
Rwanda Kinara Umri wa Kuishi Nchi za EAC
About Anonymous
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment