Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Tuesday, October 23, 2018

Wanaume Wenye Tatizo la Nguvu za Kiume Wanakabiliwa na Magonjwa Haya.


Siku za hivi karibuni serikali ya Tanzania ilipitisha aina tano za dawa za asili ambazo zitatumika kutibu maradhi ya upungufu wa nguvu za kiume, tatizo ambalo limekuwa likizungumzwa na watu wengi kutafuta suluhisho kwa waganga wa kienyeji.

Hata hivyo utafiti uliofanywa hivi karibuni unaonesha kuwa wanaume wenye tatizo la nguvu za kiume pia hukabiliwa na magonjwa mengine.

Inaelezwa kuwa wanaume wenye mbegu chache za kiume wanakabiliwa na tatizo la mafuta mengi mwilini, shinikizo la damu pamoja na mafuta machafu katika mishipa ya damu.

Kutokana na utafiti huu, wanaume wanashauriwa kuhakikisha wanafanya vipimo vya magonjwa mengine ili wawe salama zaidi.

No comments:

Post a Comment