Watu wengi hawawezi kujua harufu zao za mdomo. lakini harufu
za midomo yao ziko wazi kwa watu wengine wanaowazunguka..
Sio rahisi muhusika kufahamu kama ana tatizo hili mpaka
aambiwe na wanao mzunguka.
Mtu akishafahamu ana tatizo hili hupata hofu sana na
huathirika sana kisaikolojia kwa kuwaza kwamba jamii inamchukuliaje..
Sababu zifuatazo zinaweza kumfanya mtu awe na harufu kali ya
mdomo..
- · Vyakula na vinywaji:
Pombe na
vileo vingine huacha mabaki mdomoni ambayo huleta harufu kali ya mdomoni
pia vyakula vyenye wingi mkubwa wa madini ya sulphur kama nyama, samaki
vinapomeng’enywa sulphur hyo husafiri kwenye damu mpaka kwenye mapafu na kutoa
harufu ambayo si ya kawaida. Harufu hiyo huweza kudumu kwa masaa 12 mpaka 24.
- · Kitu chochote kinachokausha mate mdomoni:
Mzunguko wa mate mdomoni huzuia bacteria wa
mdomoni kukua .
Mdomo unapokauka mfano wakati wa kulala
bacteria hao huazaliana haraka kula mabaki mdomoni na na kuacha harufu kali
inayopatikana wakati wa kuamka.{morning breath}
Dawa pia zinazokausha mate mdomoni kama
furasamide, amitripline na piriton huweza kuleta hali hiyo.
Pia mtu anavyozidi kua mkubwa kiumri
uzalishaji wa matemdomoni unapungua na
ii ndo sababu watu wengi wazee wananuka midomo.
- · Magonjwa:
Magonjwa kama kisukari, kifua kikuu,baadhi
ya kansa, na magonjwa ya ini huleta harufu kali ya mdomoni.
- · Uvutaji wa sigara na kutopiga mswaki:
Kawaida mtu anatakiwa apige mswaki kila
anapomaliza kula yaani kama asubuhi mtu anatakiwa anywe chai kwanza ndio apige
mswaki na milo mingine ivoivo.
Pia sigara huacha mabaki yanayofanya mdomo
ue na harufu mbaya.
VIPIMO VINAVYOFANYIKA HOSPITALI:
Historia ya mgonjwa inaweza ikamfanya daktari akatambua chanzo cha harufu
ya mgonjwa kama nilivyotaja hapo juu.
Pia kuna baadhi ya vipimo huweza kupimwa
kugundua magonjwa flani. Mfano
- · Kupima kikohozi kuangalia wadudu wa kifua kikuu.
- · Kupima damu kama mgonjwa ana kisukari.
- · Uwezo wa figo na maini.{liver and kidney function test}
Wakati mwingine vipimo vinaweza kushindwa
kugundua chanzo cha ugonjwa husika.
MATIBABU:
Daktari akishafahamu chanzo cha ugonjwa ni
rahisi kuutibu kirahisi.
Mgonjwa anaweza kusafishwa kinywa na
daktari wa meno na kuanzishiwa matibabu mengine kulingana na ugonjwa
husika.{scaling}
Matibabu mengine:
·
Usafi wa
kinywa ni muhimu kwa ajili ya afya ya meno na kinywa kwa ujumla, ni vizuri
kupiga mswaki kila baada ya mlo na kumuona daktari wa meno kila baada ya miezi
sita.
Kama huwez kupiga mswaki kama hivyo ni bora ata kuosha mdomo tu na maji
baada ya kula.
·
Ulimi unaweza kusababisha harufu kali mdomoni,
hivyo usiusahau wakati wa kupiga mswaki.
·
Tumia viosha mdomo mara chache kuua bacteria
hatari mdomoni.{ mouth washes}
·
Kunywa maji mengi kama glasi nane kwa siku,
juice au tafuna jojo kuongeza mzunguko wa mate mdomoni.
No comments:
Post a Comment