Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Saturday, April 29, 2017

KUPASUKA KWA KONDOM WAKATI WA TENDO LA NDOA KUNASABABISHWA NA HAYA MAKOSA SITA.



                                                          
habari za asubuhi wadau, matumaini yangu mko vizuri na shughuli zenu..Kama tulivyosoma kwenye makala iliyopita kuhusu imani potofu zilizopo kuhusu condom,  leo somo hilo litaendelea baada ya wadau wengi kunipigia nakuuliza maswali mengi hasa kwanini condomu hua zinapasuka ovyo wakati wa tendo la ndoa,  na bila kufanya kosa nikawaandalia majibu yao kama ifuatavyo…
  • ·         Usiifungue condom yote afu ndio uivae kwani hutaweza kuivaa kirahisi na hata ukiivaa itaingiza hewa ambayo utaifanya ipasuke ndani ya mda mfupi.
  •      Usitumie mafuta yeyote ya kuongezea kwenye condom kwani utaharibu material yake ya latex na kuipasua kirahisi.
  • ·         Usitumie condom iliyobadilika rangi kwani ni dalili kwamba imeharibika au kuisha mda wake na huweza kupasuka katikati ya tendo la ndoa.
  • ·         Usitumie condom inayoonekana kukakamaa au kua kavu sana kwani inaweza ikapasuka kirahisi kwa kukosa mafuta.
  • ·         Usitumie condom mara mbili kwani inakua imeshapoteza uwezo wake wa mwanzo wa kimatumizi.
  • ·         Usianze tendo la ngono kabla mwanamke hajawa tayari kuingiliwa kwani ukavu uliokuepo huko ndani ya uke huweza kuifanya ipasuke.

No comments:

Post a Comment