Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Monday, April 24, 2017

UTI - Ugonjwa Unaoupata Kutoka Kwa Msichana Wako..

UTI - Ugonjwa Unaoupata Kutoka Kwa Msichana Wako...
Asilimia 75 mpaka 95%, ugonjwa wa UTI huambukizwa kwa kujamiiana na takwimu ya kiutaaluma, UTI ni ugonjwa unaowatokea zaidi wanawake kuliko unavyotokea kwa wanaume, kiufupi UTI ni ugonjwa wa kike ikiwa ni lazima kila mwanamke aupate katika maisha yake na kurudiwa kuumwa ugonjwa huu ni jambo linalotokea mara kwa mara.
Kwa utafiti uliofanywa na kiumeni.com, UTI ni ugonjwa unaoathiri njia ya mkojo na figo, husababisha maumivu hasa wakati wa kukojoa na pia huleta hamu ya kukojoa kwa njia ya maumivu wakati huna haja ya kukojoa pamoja na maumivu ya tumbo kwa chini. Ugonjwa huu husambazwa na bakiteria anayeitwa Escherichia Coil pamoja na fangasi sehemu za siri.
Katika dalili za mwanzo mkojo hubadilika na kuwa wa njano kama umekunywa dawa za paracetamol ambapo iwapo UTI ikikomaa kabla ya kukojoa hutoka usaa na ikiendelea zaidi husaa utakua unatoka kila mara bila kukomaa. na kwa UTI ya hali ya juu sana mkojo huchukuliwa kama sampo na kwenda kupandikizwa kwa uchunguzi zaidi, na wale wenye maambukizi ya mara kwa mara dozi ya antibiotics inashauriwa mtu anaweza kuwa anakunywa kama kinga ili kuzuia kujitokeza kwa maambukizi.

Jua Hili, Uke wa mwanamke huwa una vijidudu kinga saa zote ambapo kupungua au kuongezeka kwa vijidudu hivyo huweza kuto madhara chanya au hasi kwa afya nzima ya mwanamke, na vijidudu hivi hivi ndivyo vinavyo husika na harufu ya mwanamke inayotoka sehemu zake za siri, akiwa mchafu ndo maana anakua na harufu mbaya ndo maana mwanamke anashauriwa kuoga japo mara mbili kwa siku!. Kwa wanawake watu wazima ambao wamefikia kikomo cha hedhi wapo hatarini zaidi kupata maambukizi ya UTI kutokana na kupungukiwa na homoni ya ostrogen ambayo inausika na ute wa ukeni unaosababisha punguko la vijidudu kiga ukeni.

Maambukizi ya UTI hutokana na mambo mengi ikiwamo kwa asilimia kubwa kujamiiana,pamoja na kukojoa sehemu chafu hatarishi kwa fangasi. Ukiona dalili zozote tafadhari kapime na upate ushauri wa daktari na mpeleke mwenza wako pamoja na wewe maana ukiwa nao wewe kuna uwezekano kubwa na mwenzio anao, UTI ni mbaya na inaweza kufanya figo isifanye kazi vizuri au kuiuwa kabisa hasa kwa wale wenye matatizo ya kisukari.

No comments:

Post a Comment