Siku hizi ngono kabla ya ndoa hutazamwa na vijana wengi kama jambo la
kawaida.Vijana wa kike na wa kiume hawahisi hatia yoyote ya kuwa na
uhusiano wa kingono katika umri mdogo. Kwa kufanya hivi vijana hupoteza
mwelekeo kwa kuishi kiholela bila ya kuwa na mwongozo unaongoza maisha
yenye mafanikio sasa na baadaye. Uwezo, fursa na bahati ya vijana kwa
ajili ya maisha bora hupotea bure. Vijana hufikiria kuwa ngono ndilo
jibu na ufumbuzi wa hali ngumu wanayokabiliana nayo wakati wa balehe na
kupevuka. Wengi wao hupungukiwa uwezo wa kutabili nini kitatokea baadaye
kama matokeo ya ngono kabla ya ndoa.
Wasichana wanaojiingiza katika mahusiano ya kingono kabla ya ndoa na katika umri mdogo huweka rehani uaminifu, afya na uvumilivu wao wa hisia kuhusu mahusiano ya kingono wakati watakapo ingia ndani ya ndoa hapo baadaye.Vijana wengi hawaelewi kuwa ngono haramu huzaa wivu, tuhuma mbaya na majanga ya kijamii. Hufanya mwenzi kumfikiria msichana kuwa ana udhaifu wa kimaadili na hali hii hutia alama katika hisia za mwenzi kuhusu hali ya uaminifu wa mwenzake hasa pale anapokuwa mbali naye.
Tafiti kadha wa kadha huonyesha kuwa wasichana wasiothamini umuhimu wa kujitunza, kujilinda na kubakia waaminifu kabla ya ndoa, wana uwezekano mara dufu wa kufanya ngono nje ya ndoa baada ya kuolewa ikilinganishwa na wale wanaojitunza na kuanza ngono ndani ya ndoa. Uzoefu pia unaonyesha kuwa wasichana wengi wanaoanza ngono kabla ya ndoa, maisha yao ya baadae huwa magumu kutokana na kuacha masomo au kuzaa hovyo ovyo bila mpangilio. Wengi hujikuta wakizaa na wanaume wengi tofautitofauti na kusababisha malezi ya watoto kuwa magumu.
Wasichana wengi hufikiri kuwa ngono kabla ya ndoa ndio njia pekee ya kujenga na kudumisha uhusiano wa kimapenzi na wavulana. Hii si kweli na huenda msichana na mvulana wanaotamaniana kingono hutazamana kwa mitazamo inayotofautiana kabisa mara baada ya tendo la ngono. Ni vigumu kutabiri nini kitatokea baada ya mvulana kutosheleza tamaa yake ya ngono kwa mara ya kwanza.
Huenda mvulana akamwona msichana havutii tena kimahaba na kumchukia sana. Huenda msichana pia akapata athari za kisaikolojia na kupata hisia za kunyanyaswa kijinsia au kutumiwa kama chombo cha kustarehesha wanaume kingono. Na huenda akajichukia kwa udhaifu na kujirahisisha aliko onesha. Hii mara nyingi hutokea pale msichana anapokataliwa na mvulana baada ya kupata mimba.
Mbali na athari za kisaikolojia na kijamii, ngono katika umri mdogo kabla ya ndoa pia inazo hatari za kiafya katika mwili wa msichana. Tishio kubwa kwa wasichana ni maambukizi ya magonjwa kama vile virusi vya UKIMWI, kansa ya mlango wa mji wa mimba na magonjwa mbalimbali yaambukizayo kwa njia ya ngono.
Wasichana wanaojiingiza katika mahusiano ya kingono kabla ya ndoa na katika umri mdogo huweka rehani uaminifu, afya na uvumilivu wao wa hisia kuhusu mahusiano ya kingono wakati watakapo ingia ndani ya ndoa hapo baadaye.Vijana wengi hawaelewi kuwa ngono haramu huzaa wivu, tuhuma mbaya na majanga ya kijamii. Hufanya mwenzi kumfikiria msichana kuwa ana udhaifu wa kimaadili na hali hii hutia alama katika hisia za mwenzi kuhusu hali ya uaminifu wa mwenzake hasa pale anapokuwa mbali naye.
Tafiti kadha wa kadha huonyesha kuwa wasichana wasiothamini umuhimu wa kujitunza, kujilinda na kubakia waaminifu kabla ya ndoa, wana uwezekano mara dufu wa kufanya ngono nje ya ndoa baada ya kuolewa ikilinganishwa na wale wanaojitunza na kuanza ngono ndani ya ndoa. Uzoefu pia unaonyesha kuwa wasichana wengi wanaoanza ngono kabla ya ndoa, maisha yao ya baadae huwa magumu kutokana na kuacha masomo au kuzaa hovyo ovyo bila mpangilio. Wengi hujikuta wakizaa na wanaume wengi tofautitofauti na kusababisha malezi ya watoto kuwa magumu.
Wasichana wengi hufikiri kuwa ngono kabla ya ndoa ndio njia pekee ya kujenga na kudumisha uhusiano wa kimapenzi na wavulana. Hii si kweli na huenda msichana na mvulana wanaotamaniana kingono hutazamana kwa mitazamo inayotofautiana kabisa mara baada ya tendo la ngono. Ni vigumu kutabiri nini kitatokea baada ya mvulana kutosheleza tamaa yake ya ngono kwa mara ya kwanza.
Huenda mvulana akamwona msichana havutii tena kimahaba na kumchukia sana. Huenda msichana pia akapata athari za kisaikolojia na kupata hisia za kunyanyaswa kijinsia au kutumiwa kama chombo cha kustarehesha wanaume kingono. Na huenda akajichukia kwa udhaifu na kujirahisisha aliko onesha. Hii mara nyingi hutokea pale msichana anapokataliwa na mvulana baada ya kupata mimba.
Mbali na athari za kisaikolojia na kijamii, ngono katika umri mdogo kabla ya ndoa pia inazo hatari za kiafya katika mwili wa msichana. Tishio kubwa kwa wasichana ni maambukizi ya magonjwa kama vile virusi vya UKIMWI, kansa ya mlango wa mji wa mimba na magonjwa mbalimbali yaambukizayo kwa njia ya ngono.
No comments:
Post a Comment