Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Saturday, March 24, 2018

Ijue Sayansi ya Kupenda katika Mahusiano ya Kimapenzi


Unapoingia katika mapenzi na mtu ubongo wako unatengeneza mchanganyiko wa kemikali na kuziachia mwilini. Kemikali hizi ni pamoja na Oxytocin, Phenylethylamine na Dopamine. Kemikali hizi huongeza mapingo ya moyo na kusisimua mwili. Na hali hii ndiyo tuyoita mapenzi au mahaba.
Hali hii ni sawa kabisa na ile ambayo watumiaji wa madawa ya kulevya wanaipata.

Kama walevi wa madawa,mtu ambaye ameingia katika mapenzi anaanza kuona vitu tofauti ni uhalisia. Vitu vinaonekana ni vizuri sana na ubaya unajificha kabisa. Unaona vile vitu vizuri tu ambavyo vinakufanya ujisikie vizuri na kupuuza vyote ambavyo vinakufanya ujisikie vibaya.

Ulevi huu unakufanya uone vile vitu ambavyo wewe na mpenzi wako mnafanana na kutupilia mbali vile vyote mnavyotofautiana na vibaya.
Unakufanya pia useme na kufanya vile ambavyo vinampendeza na kumfurahisha mpenzi wako pekee.

Hali hii itaendelea mpaka kilevi kikiisha nguvu na huweza kuchukua muda wa miezi 2 hadi miaka 2. Katika hatua hii, ubongo wako unaaacha kuzalisha kemikali hizi za mapenzi na unajikuta unashangaa ilikuwaje umekuwa na mtu huyo.

No comments:

Post a Comment