Nilitulia
kidogo nikaendelea, “Moyo wangu unasononeka sana. Laiti ningelijua
nisingeoa, maisha gani haya yananitesa kiasi hiki?”Nilijikuta nikilia
ovyo kama toto jinga lenye kudeka ovyo.Kilio changu lilikuwa rohoni.na
aliyejua alikuwa muumba pekee.Getruda alikuja kunibembeleza kwa hofu
kwamba ningechukua maamuzi ya kijinga tena. Aliniandalia chakula
mezani.Tulisali kisha tukala .
Saa
nane mchana baada ya kupata mlo wa mchana nilimuaga Getruda nikiwa
naelekea ofisini kumueleza Mzee Jophu yaliyosibu katika unyumba wangu.
Lakini cha kushangaza Mzee Jophu baada ya
kumueleza kila kitu,nilimuona uso ukiwa umejawa furaha badala ya
kunionea huruma. Hali hiyo aliisubiri kwa hamu hata hivyo alishanga kuona mimi kuchelewa kumuelezea shida zangu toka mwanzoni.Alijifanya kama hataki kuchangia mapenzi ilinimuone mtu mwema,
“Sasa Jophu unakataa nini na wakati nimekuambia mke wangu hajaguswa”
“Inamaana siku zote hizo mlikuwa mkilala tu?”
“Ndio”nilimjibu nikahisi machozi yakinilengalenga, hata hivyo nilijikaza kiume.
“Matatizo haya yalikupata muda gani?”
“Siku ya kwanza toka nifunge ndoa na mke wangu”
“Usinitanie Sweedy. Ulijaribu kwenda hospitali?”
“Ndio.Nilichunguzwa
kwa makini.Daktari alinieleza kwamba nilipigwa sindano yenye
sumu.Nilikataa kwani sijawahi kupigwa sindando yeyote toka uliponiajiri.
Na sasa ni miaka karibu ishirini na tano. Nakumbuka sindano ya mwisho
nilichomwa nikiwa na chuoni. Na siku nyingine niile nilipokuja kutolewa damu”
“Kutolewa damu si kupigwa sindano labda una matatizo mengine kiafya.Vipi kuhusu chango?”
“Sina chango,mzee”Nilimjibu nikiwa nimetizama chini.
“Mzee,
naomba unisaidie kuokoa jahazi la ndoa yangu”Nilimweleza nikimpigia
magoti.Sikuwa najua kwamba mzee Jophu ndiye aliyetuma watu wanipige
sindano ya kuua uume wangu.Wakidai wana nitoa damu ilinikapimwe virusi
vya ukimwi.Hata hivyo ilikuwa kazi kumgundua mbaya wangu,jinsi
alivyoonyesha kutokutaka kuchukua jukumu la kumridhisha mke wangu.
“Mkeo atakubali kwenda kupima damu zetu?”
“Sina uhakika kama atakubali au laa. Ni vizuri kimpigie simu”Nilitoa simu yangu ya kiganjani na kubonyeza namba za Getruda, mke wangu.
“Hallo, mpenzi”alipokea tu baada ya kuona namba zangu juu ya kioo cha simu yake.
“Oooo!, vipi upo salama.”
“Ndio. Sijui wewe”
“Shwari kabisa.Mmmm…utakubali kupima Virusi vya ukimwi?”
“Tangu lini kigori akawa na Ukimwi?”
“Sijambo la ajabu kwani ukimwi unaambukizwa kwa kujamiana tu?”Getruda aitafakari akajiona kweli alibugi sana.
“Sawa, nimekubali kupima afya kwa manufaa yetu sote”
“Ok, jiandae nakuja sasa hivi nyumbani”
“Ok, bye bye”Alinaga na kukatasimu.
“Nilimtizama mzee Jophu na kumwambia, “Amekubali kupima”
Kwambali niliona tabasamu la mzee Jophu lililonifanya nione meno yake ya rangi rangi, nafikiri kutokana kunywa maji ya Arusha tokea utotoni mwake.
“Sasa
Sweedy”Alitulia kidogo na kukohoa kinafiki,nilimtizama kwa makini
niwezekujua alichotaka kusema,aliendelea “Kwa vile wewe ni rafiki yangu
sina budi kukusaidia.Ila nakuomba usimweleze mtu yeyote ‘Especial my
wife’,Umenielewa. Narudia tena naomba iwe siri moyoni mwetu”
“Sawa, mzee.Usihofu kitu”nilimjibu kwa upole kabisa.
Mzee
Jophu aliongea moyoni akiwa amejawa furaha kubwa mno, “Kile
nilichokitaka kimekamilika. Sasa kazi kwangu kurina asali nitakavyo””
Mzee
Jophu kunajambo la muhimu nimelikumbuka. Nilimdanganya kuwa
nilimwagikiwa na tindikali. Akikuuleza mueleze ni kweli”Nilitulia
kidogo, ingawa alijaribu kuficha furaha niliiona , Nikatulia kama
niliyewaza kitu ,Machozi yakaniwakia pale nilipokumbuka nguvu zangu
nilipokuwa Nchini Thailand “Lakini boss na shindwa kujua ugonjwa huu
niliupata wapi na nani aliyeniletea”
“Usijali
muombe mungu akuondolee. Hatamimi ninafanya tu, kwa vile wewe rafiki
yangu wa damdam, lakini kwa maulana ni dhambi kuzini nje ya ndoa,” Mzee
Jophu aliongea ilinimuone mtu wa busara kama alivyoonekana kuwa
ni mtu wa busara kumbe ni muungwana wa ngozi tu, lakini rohoni ni
muuwaji. Maneno yake ilikuwa vigumu kumgundua kuwa yeye ndiye mbaya
wangu, aliyeamua kunitesa iliamfanye mke wangu wake.
Mazungumzo
yetu ya ofisi yalikuwa ya muda mrefu. Tulipo maliza jioni iliwadia
tuliongozana na Mzee Jophu moja kwa moja hadi nyumbani kwangu.
“Lakini Sweedy kama ameoa mke mwenye uso wa mbuzi mimi sitamkubali atakuwa wako mwenyewe”
“ Hakika mke wangu utamkubali. Amekamilika kila idara. Utamsahau mama Jacob nakuambia” Nilimueleza.
“Yote tisa, kumi tutaona. Nitaamini unajua kuchagua,”
“Lako
jicho, yanini ni kusifie?” Niliposema, nilitamani Mzee Jophu ardhike na
ombo la Getruda, lakini kitu kilichoniuma zaidi ni jinsi gani
ningemuunganisha mwanaume mwenzangu na mke wangu niliyemlipia mahari.
“Inawezekana huyu mshenzi akamkataa mke wangu. Midomo yake imejaa dharau”nilijisemea kimoyomoyo huku nikibonyeza kitufe cha geti.
Getruda
Kimario alifika getini na kufungua, mtu wa kwanza kuingia akiwa Mzee
Jophu.Shauku yake haikufichika ,alimtupia Getruda jicho la lilo jaa
ubembe.Ni hapo ndipo nilipohisi Mzee Jophu kumkubali mke wangu. Alikuwa
na shauku ya kumbusu Getruda, nikipindi kirefu toka wapoteane pale
ofisini kwake, na Getruda alimkumbuka kuwa yule alikuwa yule aliyempa
mama yake mzazi shilingi laki tano za kitanzania iliamuowe yeye.
Walitupiana macho yaliyojaa furaha macho ya matamanio ya Getruda
yalizidi kumchanganya Jophu. Aliyekuwa na shauku kuupitisha usiku
mwanana na binti aliyemlipia shilingi laki tano. Aliamini alikuwa na
haki yakujivinjari jasho lake.
Mwanzoni nilihisi hawakumbukani,kumbe kumbukumbu alikuwa nazo na alishuhudia mama yake akipokea hizo hela.
Ulifikia
muda muafaka wakuweka mambo hadharani ili nitatuliwe shidayangu. Kabla
sijazungumza chochote nilipandisha pumzi na kushusha kwa nguvu kama mtu
aliyechoka na pilika pilika za kutwa nzima
,”ooooooophhhh!”Kisha nikasema kwa sauti ya chini kama mgonjwa,ni kweli
niliyotaka kusema yaliniuma sana.
“
Nafikiri mke wangu nilisha wahi kukutajia jina la rafiki yangu kipenzi.
Ila ni vema nikalirudia leo ukiwa una muona . Aliye kaa hapa mbele
ndiye Mzee Jophu. Sio Mzee kweli ni kwaajili ya mali zake ndio maana
watu wanampa jina la heshima ya mzee. Huyu ndiye
mwa ndani wangu ukimuona yeye ndio umeniona mimi. Shida zake ni zangu,
zangu ni zake,”Nilikohoa kidogo ni kumgeukia mzee Jophu. Kijasho
kilizidi kuchuruzika kwa kasi kuliko mwanzoni, nilihisi midomo kufa
ganzi na kuwa mizito, nilijikuta sauti ikipotea ghafla pale
nilipofikiria kumuachia mzee Jophu mke wangu.Tena hajawahi kuguswa na
mtu yeyeto maishani. Kwa kweli inatia uchungu sana heri ningekuwa nimezaliwa na udhaifu huo kuliko kunikuta nikiwa mtu mzima.
“Mzee
Jophu huyu ni mke wangu, kwa upande mwingine naweza kusema ni mkeo.
Nina matatizo ya,,,,,,” hasira kali iliniingia moyo nikashindwa
kumaliza, nilijikuta nikiangua kilio. Moyo uliuma sana.
“Kweli
kweli na muachia Jophu kigoli wangu?”Nilimtizama Getruda kama vile
nikimuaga, sikuweza kukwepa jambo hilo tena.Kwa kuwa lilishakuwa kero
katika familia yetu.
“Naomba
uwe karibu na mke wangu, kama ulivyo karibu na mkeo,
lakini,,,,,,,,,,naomba unifichie siri yangu, heshima iwepo msije
mkachukulia muda huo kunidharau, nami sikupenda kuwa
hivi,,,”Nilikokoteza maneno kwa ujasiri .
“Ok,
nashukuru kumfahamu mkeo, na nitaendelea kumfahamu vizuri, zaidi kadri
siku zinavyo zidi kwenda” Mzee Jophu aliongea huku akinyanyuka kuelekea
alipo Getruda. Alinishika mkono na kuunyanyua usawa wa midomo yake,
hakuchelewa nilisikia sauti ya busu kwenye kiganja cha mke wake wangu.
Busu hilo lilimchanganya mke wangu na kujikuta mwili ukimsisimka,
vinyweleo na nywele zilisimama kwa shoti ya busu la mzee Jophu.Nilibaki
nimeduwa, midomo ikiwa wazi kama sekunde kadhaa.Bila hofu wala haya,
walijikuta wamekumbatiana na Mzee Jophu alisogeza midomo yake karibu
kabisa na sikio akimnong’oneza.
“Kweli
kwenye miti hakuna wajenzi, nitakutunza kama mlima Kilimanajaro
unavyotunza Seluji yake, nitakupa chochote unachotaka, ikiwezekana
nitakuoa kabisa, nakupenda siko tayari kukuacha, naamini unanipenda”
Sauti ya Mzee Jophu ilizidi kumtekenya Getruda, alijikuta akitikisa
kichwa ishara ya kukubali.Alishindwa kujizuia kutoa sauti za kizizima,
taratibu kwa jinsi maneno ya Jophu yaliyokuwa yakipenyeza sikioni angali yana uvuguvugu, kwa wimbi lenye joto nadhifu.Mzee Jophu alimwachia na kuketi karibu nae.
Mambo
yote niliyaona. Kwa jinsi roho ilivyoguguna niliondoka sehemu ile na
kuingi chumbani, nilimpenda sana mke wangu, sikupenda awe mke wa shirika
wala sikupenda kuona akishikwa shikwa na mtu zaidi yangu. Japo nilikuwa
na wivu lakini nilishindwa kwa sababu nilipata udhaifu, ikanilazimu
kuvumilia na kuhamisha macho, na kutizama pembeni.Pia hilo lilinishinda nikaamua kujiondokea kiunyonge kama kifaranga asiye na mama.
No comments:
Post a Comment