“Kuna
rafiki yangu mpenzi ambaye tupo karibu .Yeye ndie mwandani wangu, siri
zangu ni zake na zake ni zangu nitamueleza kilio changu. Naamini
atakisikiliza na kulichukulia kama kilio chake na atanisaidia shida
ndogo ndogo za unyumba wetu. Mtu huyo ni tajiri yangu anayeitwa Mzee
Jophu. Itakubidi unihifadhie aibu hii moyoni mwako. Ndiye ambaye siku
ile ulivyoletwa na Baba niliwaacheni nae nikiwa na maongezi ya faragha
na Baba.” Nilijaribu kumueleza mke wangu kuwa pengine angekubali
kutembea na rafiki yangu mkubwa badalaya ndugu , na aendelee kinitunzia
heshima yangu kama mumewe. Japo roho ilikuwa inauma kumkabidhi mwenzangu
boma langu. Wala sikuweza kugundua kuwa mzee Jophu ndiye aliye panga na
Daktari anipige sindano ya sumu.
“Kama
una matatizo ndoa ya nini?.Suluhisho ni kuivunja ndoa kwa amani sitaki
kujidhalilisha kwani wanaume wameisha duniani? Isitoshe nilishakutaarifu
kwamba sijawahi kuguswa, bado nina nafasi kubwa
ya kuolewa, wameolewa machangudoa sembuse mimi kigoli. Siwezi kukuelewa
kabisa ninachotaka ni talaka yangu. Kuishi na wewe ni sawa na
kulinganisha kifo na usingizi” Mke wangu alinibadilikia ghafla, sikuweza
kuamini maneno hayo yaliyotoka kinywani mwake . Hali hiyo ilininyima
amani na kijikuta nikilia kama mtoto mchanga aliye hitaji ziwa la mama
yake baada ya kulikosa kutwa nzima bila kunyonya.
“
Sijali kulia kwako kwani mimi ndiye niliye kumwagia tindikali? Mlaumu
aliye kumwagia na sio mimi.Kweli ving’aavyo vyote si dhahabu. Najuta
kuolewa na watu waliochelewa kuoa, huenda ni matatizo uliokuwa nayo toka
zamani”. Getruda alizidi kuniumiza moyo.
“Sawa
najua sina faida ya kuishi duniani,nitawaachia ninyi wenyewe umuhimu na
hii dunia, lazima nife …….sio muda mrefu utaniita marehemu sio Sweedy
tena ,” Nilijikuta shetani mbaya akiniingia kichwani na kuiteka akili
yangu, nikaamua kujiua tu, sikupenda kuishi na mateso. Niliondoka na
kuingia chumbani kwetu, nilijifungia kwandani na kutafuta kamba tayari
kutoa uhai wangu. Nilikusudia kujiua na niliamua kufanya kama mawazo
yalivyo nituma, sikupenda kuishi kwa manyanyaso, mateso ya unyumba.
Nilikuwa
chumbani na tafuta kamba ya kujinyonga, Getruda, mke wangu muda mfupi
tu, angeniita marehemu badala ya Sweedy. Getruda akiwa kwenye mtiririko
wa mawazo alisikia sauti yangu, (LORD YOU KNOW MY TRIBLES)” “Mungu
unajua mateso yangu”Wakati nasema maneno yale ,nilishafunga kitanzi juu
ya paa la numba.Nilikuwa nimepanga stuli mbili zikiwa
zimebebana,nikaanza kuingiza shingo kitanzini,
nilihakikisha kamba haitakatika. Iliyofuatiwa sauti nyingine nikimuaga.
“Getuuuuu! Kwa heri niagie ndugu wote, nimeamua kufa sipotayari
kunyanyaswa na udhaifu wangu, hata mungu anajua”. Taratibu nilianza
kusukuma stuli nilioikanyaga ili idondoke na nijinyonge, Muomba kifo
hakosi basi stuli ilidondoka kamba ikaninyonga.
“Ahiiiii”nilitoa sauti moja kwa shida sana.Kutoa neno la zaidi,nilijijigeuza na nikawa natapatapa kama mfa maji.
“Haraka
Getu aliamka na kuekekea sauti ilipotoka, aliamini nilikuwa nianajiua
akajuta na kujilaumu kwanini alinipa maneno ya ukali badala ya
kunifariji.
“Dhambi zote ni mimi, isingekuwa mimi asingejiua, yanipasa nijitahidi kumnusuru na kifo,” Getu alianza kuniita
kwa sauti ya huruma, “Sweedy…Sweedy… naomba unisikilize mkeo naongea.
Niwie radhi nilikuwa na kutania nimekubali kuwa na rafiki yako. Naomba
unielewe mpenzi nitalitunza penzi lako na siri yako. Kama nikujiua basi
nisubiri tuongee nitakuacha uendelee kujiua.” Getu aliendelea kuniita
bila ya kupata kujibiwa. Kilikuwa kitendo cha haraka alichukua uamuzi wa
kuvunja mlango na kuingia ndani, alinikuta nikiwa nimeningia mapovu ya
kitoka puani.Aliona kisu kilichokuwa mezani,Hakupendakupoteza muda ,kwa
mwendo wa umeme alikata kamba na nikadondoka chini kama
gunia la maharage, aliponigusa alipeleka mkono kifuani kuona kama
nilikuwa hai. Ajabu ni kwamba hakusikia mapigo ya moyo ya kienda. Miguu
ndio ilikuwa nikiitupatupa huku na kule, ulimi ukiwa nje kama wa kenge.
Hali iliyomfanya asijidanganye kuwepo hai tena na kuamini zisingepita dakika kumi ningepoteza uhai.
Uzito
wangu haukuwa kigezo kikubwa cha kumfanya Getruda ashindwe kunibeba,
alijitahidi alivyo weza kunitoa nje ambako alipiga simu kwa dereva teksi
aliyemfahamu. Dakika takribani mbili ,alisikia gari likiegeshwa nje ya
jengo letu.
“Vipi shem. Imekuwa je?”Dereva teksi aliuliza.
“Wee achatu.Hebu tumuwahishe hospitali mazungumzo baadaye”
Walinibeba
juu juu hadi kwenye gari, dereva akafungua mlango wa nyuma ambako
walinilaza chali na kufunga mlango.Hawakukawia kufika hospitali ya rufaa
Mount meru kwa matibabu zaidi.Getruda aliniingiza ofisi ya dakitari wa zamu.
“Anasumbuliwa hasa na nini?”
“Amevamiwa
na majambazi ambao walimnyonga kwa kutumia kamba”Getruda alidanganya
wazi wazi.Huku akiuma mdomo wa chini kana kwamba alijawa na dhahabu
kali.
“Sasa umeripoti polisi?”
“Daktari mbona unaniuliza maswali ya sio na msingi kabisa.Wewe unataka ripoti ama kumtibu mgonjwa?”
“Hatuwezi kutibu bila kupokea karatasi ya PF3 kutoka polisi”
“Dokta kipi bora .Kuokoa maisha ya mgonjwa ama kumwacha afe kwa sababu ya PF3?”
“Kuokoa maisha yake”Dokta akajibu akichukua vipimo vyake.
“Basi kumbe unajua. PF3 baadae, nisamehe kama nimekuudhi”Getruda alimwomba radhi Dokta.
Dokta
alinishughulikia kwa haraka.Nilitibiwa kwa makini na baada ya saa nzima
nilipata ahuen.Ila kooni nilihisi maumivu kwa ndani.
**********
Zikawa zimepita Siku mbili toka nilipookolewa na Mke wangu,Getruda pale nilipokuwa najiua kifo cha taabu.
“Mume
wangu nilikuwa nikikutania . Tafadhali usijaribu kujiua tena.
Nimekubali mlete huyo rafiki yako leo nimuone kama sura yake ina tapisha
au laa!” Getruda hakupenda kufanya hivyo aliamua kukubali ili
kuninusuru kifo. Sauti ya Getruda ilipenyeza kwenye ngoma ya masikio
yangu fundo kali la sononeko liliingia moyoni.Nikajivuia kulia kwa nguvu
zote lakini nilijikuta machozi yakichuruzika taratibu bila kujua.
“Sawa mke wangu utamuona nitakapomleta jioni,” Ilikuwa asubuhi na mapema, majira ya saa moja na nusu.
“Mmmm! Lakini Getruda unanipenda.Isingekuwa wewe basi nilikuwa mfu”Nilimweleza Getruda.
“Kumbe unalijua.Mkojo ulishaanza kukutoka”
“Masihara hayo.Inamaana nilikikojolea kama mtoto”
“Ndio”Getruda alinijibu akainuka kitini na kuelekea kwenye jokofu ambako alilifungua na kunipatia Juisi baridi ya machungwa.
“Karibu mpenzi”
“Ahsante
mpenzi”Niliipokea na kumtolea tabasamu,lakini nilipokumbukla kwamaba
nahitajika kumtambulisha bosi wangu.Moyo ulisingaa na kunyauka kama jani
la tumbaku lililosubiri kusagwa.
“Mpenzi nataka kwenda kujipumzisha kidogo”
“Sawa,ila
usisahau kwenda kumleta rafiki yako jioni”Nilishituka na kutulia kama
sekunde kadhaa ,kisha nikageuka kumtizama mke wangu.
“Utaniamsha baada ya saa moja.
Ok,
bye”Nilijikaza kutoa tabasamu ambalo pengine lilionekana dhahiri la
kulazimisha, huku moyo ukiniuma kama kutu inavyokula chuma taratibu na
kukiozesha chote.
“Nije tujipumzishe wote?”Getruda alinieleza wakati nikiwa nimempa mgongo.
“Poa. Ukipenda”Nilimjibu damu zikienda mbio ,ungeweza kuhisi nimekimbia umbali mrefu bila kupumzika.
Getruda alinifuata chumbani kama alivyoomba.Nilijitupa
kitandani kiuvivu uvivu nae akajibweteka kwenye sofa moja lililomo
chumbani.Ingawa nilifumba macho lakini sikuwa hata na lepe la usingizi,
mawazo yangu yalimezwa na taswira ya maisha ya unyumba.Nilijiuliza bila
kupata jawabu sahihi kwamba ugonjwa huwa niliupata wapi na nani
aliyenipa?.
Nikiwa
nimelala nilihisi vidole laini zikitalii mwilini mwangu.Hata hivyo
sikushituka kwani nilihiosi alikuwa mke wangu.Vidole hivi vilizunguka
huku na kule bila kupumua,nilihisi kama kero ama mdudu fulani
akinitembelea akini kwarua. Sikuona raha zaidi za mateso tu.
“Hallo Sweedy”
“Na..a.amu”Nilikokoteza maneno,nikiwa nimetulia utadhani mbwa anayetolewa kupe.
“Unanipenda?”
“Saaana tu”
“Kwanini hunipi haki yangu kama kweli unanipenda?”
“Haki ipi?.Si una jua matatizo yangu sasa unataka nini tena”
Nilihisi Getruda akinitibua akili yangu.Niliinukla na kutoka nje.
“Getruda unanitesa. Tumepanga nini na wewe unataka nini?”
No comments:
Post a Comment