Kesho
yake ilikuwa siku ya mimi kupimwa afya ikiwemo na kupimwa virusi vya
Ukimwi, sikuwa na wasiwasi nilisubiri waje kunipima kwani nilijiamini
sikuwa na virusi, japo nilifanya mapenzi na Jennifer kule Thailand bila
kutumia kinga yoyote.Na hata mapenzi niliyofanya yenyewe yalimfurahisha
na kumridhisha Jennifer na kukiri mimi ni miongoni mwa wanaume wanaojua
mapenzi. Sikupenda Jennifer anidharau kwa upande wa kutomridhisha
kimapenzi.
Waliingia
Daktari waliovaa magwanda meupe wakiwa na vipimo vyao. Waliongozana
moja kwa moja ofisini kwangu, cha ajabu baada ya kusalimiana nao
walitaka nivue nguo nibaki na kaptula, jambo hilo nilipinga.
“Kama kunipima damu ninatolewa damu kwenye mkono sio karibu na uume wangu. Nyie ni daktari kweli?”
“Ndio sisi ni daktari unataka vitambulisho?”.
“Sina
shida na vitambulisho vyenu. Nyie chukueni damu mkaipime, mkileta
majibu mabaya nitarudia hospitali nyingine niliwaeleza waziwazi bila
kuwaficha kitu.”Nikiwa nimeketi kitini,wao walikuwa wamesimama.
Haraka
haraka daktari mmoja alitoa sindano iliyokuwa na kitu kama maji, sijui
ilikuwa sumu au ilikuwa nini!. Maji hiyo ilikuwa ndani ya bomba la
sindano. Kama cc 200. Sikuweza kuona nilikuwa nimegeuka kwa upande
mwingine ili nisione sindano inavyopenya na kuingia kwenye nyama za
mwili wangu. Kwa kifupi nilikuwa muoga wa sindano japo nilikuwa mtu
mzima.
Wakati
sindano ipo kwenye mshipa wa damu nilisikia kitu kama maji yenye
uchungu wa dawa, nilipata maumivu makali nilipogeuka ndipo niliona
akigandamiza bomba la sindano kwa haraka ili nisione kitu, lakini
niliona kitu kilichoingizwa kwenye mshipa wa damu. Nilishindwa kujua
kilikuwa ni kitu cha kuniletea matatizo ama kunijenga ndani ya mwili
wangu.
“Dakitari
wewe unanipiga sindano au umekuja kunitoa damu ili upime Virusi vya
Ukimwi?. Iweje unipige sindano?”. Nilimuuliza daktari kwa hasira baada
ya kusikia ile sindano mwili mzima, nilihisi kizunguzungu mwili ukakosa
nguvu. Tofauti na kabla ya kuingiza sindano yao, halafu walikuwa bado
hawajatoa damu.
“Usijali Sweedy sijakupiga sindano, nataka kutoa damu” alisema huku
akivuta damu kwenye bomba la sindano. Na muda mfupi waliniaga,
alionekana nesi mmoja kati ya wale waliokuja kunitoa damu mwenye
majonzi. Alinitazama kama mtu aliyenionea huruma sana, machozi
yalimlenga lenga lakini hakutaka niyaone aligeuka upande wa pili na
kujifuta na kitambaa alichokuwa nacho mkononi. Nahisi alikuwa anajua
kila kitu kilichotendeka kwa muda ule na sura yake ilikuwa sio ngeni
machoni mwangu, lakini nilishindwa kumkumbuka vizuri. Alijua mipango
yangu yote hasa ile ya kufunga pingu za maisha. Alijaribu kuwa wa mwisho
kuniaga.
Nilisikia
akiniambia “Pole sana Sweedy, moyo unaniuma Mungu akubariki maishani.
Nenda kanywe maziwa mengi yatakusaidia”. Nesi huyo aliondoka taratibu,
huku akigeuka nyuma na kunitazama kwa macho ya huruma. Nilishindwa
kumjibu, nilibaki nikiyaganga maumivu ya sindano niliyochomwa mara ya
kwanza, ambayo sikuweza kuielewa ilikuwa ya nini mwilini mwangu.
Robo
saa baada ya wale daktari kuondoka mkono niliopigwa sindano na kutolewa
damu nilihisi unakufa ganzi, kila nilipotafakari yale maneno ya yule
nesi na kilio chake nilishindwa kumuelewa zaidi ya kujilaumu kwa nini
nimekubali kupimwa pengine wamenipiga sindano yenye sumu ambayo
itanidhuru. Kwa upande mwingine sikuamini niliona yule nesi alinipenda
bure, na Mzee Jophu asingeweza kuwatuma watu wanipige sindano yenye sumu
. Nilimuamini sana tajiri yangu.
****************
Wiki
tatu zilitimia na siku ile ya harusi iliwadia. Kila mtu aliisubiri kwa
hamu sana siku hiyo hasa wazazi wangu kwani walijisikia furaha kwa mtoto
wao wa kiume pekee kufunga pingu za maisha. Nadhani moyoni mwao
walijisemea, sasa ule wakati wa kuwaona wajukuu toka kwa mtoto wetu
Sweedy umewadia. Mzee Jophu ndiye alikuwa mtu wa kwanza kwa watu
walionichangia mchango mkubwa katika kuifanikisha harusi yangu. Sherehe
ilipendeza sana, watu walikula na kunywa hadi wakasaza. Namshukuru Mungu
sikupata lawama yoyote ya kuhusu sherehe yangu.
Getruda
ambaye ndiye ubavu wangu sasa aligubikwa na furaha isiyo kifani.
Sherehe iliyopendeza kwa shamrashamra na vifijo, DJ alitumbuiza kwa
muziki wa taratibu wa wapendanao hasa kibao kilichopigwa na mwanamuziki
Bob rudala nadhani msomaji unaupatapata ule wimbo vilivyo . Utajisikia
vipi ukipigwa siku ya harusi yako? “NIMEKUCHAGUA WEWE” nakumbuka baadhi
ya maneno yake, “Nimekuchagua wewe uwe wangu, wangu wa maisha wa kufa na
kuzikana”msomaji sitaki nikumalizie uhondo tafuta wako na wewe awe wa
maisha ili ujiepushe na mengi hasa janga la Ukimwi. MC au Msema chochote
watu wa mjini wanavyoita alikuwa anaitwa MR.Kicheche ni kicheche kweli
si mchezo ukumbi haukuruhusiwa kukaa kimya siku hiyo watu wote walikuwa
wakicheka na kutabasamu kwa wale wasio na bandama. Kwa ufupi sherehe
ilipendaza mno, hatukuwa matajiri lakini watu wailiridhika na kila idara
ya sherehe.
Sherehe
ilipoisha, tulichukuliwa na gari maalumu siku hiyo kwa bwana na bibi
harusi na tukaelekea kwenye hotel moja iliyoitwa NGORONGORO HOTEL
kujipumzisha. Tulipofika tulikwisha andaliwa kila kitu, chumba kilinukia
harufu nzuri za manukato, choo na bafu ndani kwa ndani ilipendeza kwa
kweli. Washenga waliondoka tukabaki mimi na mke wangu Getruda Kimario.
Nilikuwa
na shauku kubwa ya kukabiliana na binti ambaye alikuwa kigoli, ambaye
hakuwahi kuguswa, nilitamani kupata ukweli wa maneno ya baba
aliyenieleza kuwa mke niliyeoa alikuwa bikira, na mimi nilitamani kumtoa
mwenyewe yaani kama ni gari lilikuwa jipya ‘New model’ na sio mtumba.
Tuliongozana
bibi mbele bwana nyuma, wote tukiwa tumefunga taulo tuliingia bafuni na
kuanza kuoga. Kweli uzuri wa mke wangu niliufananisha na lulu au tunda
Apple. Alikuwa na umbo dogo lenye figa, ambalo lilinifanya nimtamani
zaidi na zaidi. Si kifuani, usoni na umbo lote lilinivutia sana.
Nilimuogesha nae aliniogesha, tulipomaliza tulijifuta na taulo na
kuelekea chumbani.
Tulijitupa kitandani, “Samahani mpenzi nikumbatie, nahisi baridi…nahitaji…..” Ilikuwa sauti ya Getruda iliyojaa mahaba na iliyonisisimua mwili na kuhisi joto .
“Usihofu
kila kitu kitakuwa shwari, nitakupa kila kitu unachokitaka” nilimjibu
kwa sauti nzito iliyomuingiza kwenye ulimwengu wa mahaba.
“Lakini mpenzi unajua nakupenda sana” Getruda aliongea macho ya udadisi yakiwa yametuwa usoni mwangu.
“Naamini
unanipenda mke wangu ndio maana ukaamua tuoane, lakini nahisi mimi
ndiye nimezimika kwako zaidi” nilimweleza na hapo hapo tulikumbatiana na
mabusu motomoto yalishamiri, si mashavuni, mdomoni na kwenye paji la
uso kote tulipeana mabusu ya upendo.
Niliyasikia
mapigo ya moyo wake yakienda kwa kasi jasho jepesi lilimchuruzika
taratibu nilishindwa kuelewa kwani AC au ‘kipupwe’Kiyoyozi kwa jina letu
la kiswahili kilikuwa kinafanya kazi yake kama kawaida. Kila
nilipomshika kwenye kona za mapenzi nilimsikia akizizima kwa sauti za
mahaba, si kwikwi wala kuweweseka zote zilimburudisha. Niliamua kutulia
kidogo baada ya kuona mambo yote nilikuwa namfanyia uume wangu
hausisimka hata kidogo, tofauti na siku za nyuma busu moja kila kitu
kimesisimka, leo mambo yote sikuona hata dalili.
“Oooh.!!! Sweedy unajua mimi sijawahi kuguswa kabisa!”
“Eti!, samahani sijakuelewa mke wangu”
“
Sijawahi kufanya mapenzi toka kuzaliwa. Naomba unifundishe” sauti
nyororo na ya simanzi ya Getruda ilinifanya nilie mwenyewe, sikuwa na
nguvu za kiume, bali nilitamana kumkabili mke wangu nilishindwa kujua
Ugonjwa wa kupooza kwa uume wangu ulitoka wapi na nitamuambia nini mke
wangu, na je atanielewa na wakati nishamchezea kila sehemu, nilizidi kulia sikuwa na la kufanya.
“Unalia
nini tena mume wangu?” Getruda aliniuliza akiwa kalala chali, kama
mgonjwa aliye mahututi . Mweupe mwili wake ulipendeza na kuzidi kung’ara
kila nilipomtazama usiku ule, kwa ufupi alikamilika kila
idara,nilitamani nimrukie lakini jogoo wangu hakutaka kuwika kabisa.
Nilidanganya “Mke wangu nimeshikwa na kichomi cha tumbo sijui ni hiyo AC
“kipupwe” niliongea kidhaifu nikiwa nimeshika tumbo, machozi
yakiendelea kuchuruzika taratibu, niliamini kwa maneno ya kusema
“Naumwa” Getruda angeridhika na kunionea huruma, aliniangalia kwa huruma
na kusema
“Basi mume wangu tuzime usije ukapata matatizo zaidi”. Nikaona duh! Acha nizidi kujitetea “Labda upunguze kidogo”Nilisema nikiwa nimekunja sura na kushika maeneo ya tumbo.
“Pole mpenzi” mke wangu alisema kwa sauti ya utulivu.
“Usiku huu tutapata wapi dawa?. Jikaze usilie”Mke wangu alinionea huruma.
“Usijali mama watoto.Huwa natokewa na tatizo la kichomi ninapofikia hatua ya kufanya tendo la ndoa”
“Kwa hiyo utafanya je?”
“Daktari aliniambia tatizo hili litaisha baada ya kuzoea mwanamke”
“Mwanamke gani, mbona sikuelewi?”
“Wewe,
Usijali tatizo hili litaisha”Nilizidi kumpa motisha mke wangu.Lakini
moyoni bado wasiwasi ulitanda kuhusu jambo hili geni kabisa mwilini
mwangu.
Maneno
hayo ndio yaliyomfanya Getruda, mke wangu ainamishe kichwa magotini
mwangu kama mtu aliyekuwa akisujudu. Sikujua aliwaza nini akilini mwake,
lakini nikahisi yote yalikuwa juu ya matatizo niliyonayo.Muda wa dakika
takribani tano nilihisi kitu kama maji maji angali yenye uvuguvu
yakidondoka gotini kwa tone moja na moja.Matone hayo nilihisi ni machozi
,nikaamua kuinua uso wake kutizama kwamba ni
nini hasa.Kila nilipojaribu kumuinua alikaza shingo.Wazo ambalo nilihisi
kwamba alikuwa akilia likajidhatiti akilini na kuhisi sikukosea.Pia
nilijaribu kwa mara nyingine kumuinua uso wake, safari hii akanisemesha
akionekana kukasirika.
“Mume
wangu umeamua kunitesa angali unajua unamatatizo. Kwanini usingenieleza
kabla, umenitesa naunaendelea kunitesa. Utafanya nini ilikunisaidia,
najisikia vibaya sana mwenzio” aliongea kwa sauti ya chini akiwa
anadondosha machozi, mwili wake ulikuwa umelegea, macho mekundu na ya
kurembua, hakuweza kuvumilia zaidi ya kulia kwa kwikwi, alitamani
niondoe hali ya ubikira na kumpeleka kwenye utu uzima. Maneno ya Getruda
yaliniumiza moyo wangu, nilimuonea huruma alivyokuwa akijigaragaza
kitandani. Machozi yalichuruzika kwa kasi nilizidi kuwaza.
“Au
ni kwa vile ndio mara ya kwanza kukutana naye nini?. Lakini hapana
sijapaniki” labda ni uzuri wake unanichanganya nini? . Au ni chango la
tumbo limesababisha nini?.Sasa tatizo hili litaniumbua” Nilijiuliza bila
kupata muafaka wala sikuweza kuhisi kitu chochote zaidi ya ugonjwa wa
kawaida. Tuliupitisha usiku huo usio na ladha ya mapenzi, si mimi wala
Getruda wote tulihuzunika.
No comments:
Post a Comment