Nilionekana
kuchanganyikiwa badala ya kuingia chumbani nilijikuta naingia chooni
nilistuka ndipo akili ilipo rejea vema. Nilichomoa bastola yangu na
kuelekezea mbela tayari kwa vitachumba walichochukua kilikuwa cha mwisho
kabisa. Nilipokaribia chumba, nilisikia sauti za kilio kikubwa chumbani
humo.
“Oooooo! Jophu unaniumiza unaniua jamani!niachecheeeee!…nakufa!”Sauti ilikuwa nzito ilioitikia
“Tulia
mpenzi niku………kuku…….tengeneze.Unana……najua….wewe ..ni mzuri sana
lazima nikuoe”Mzee Jophu alikokoteza maneno kwa kigugumizi kikali akiwa
kifuani mwa Getruda.
Sauti
hiyo ilinilegeza viungo,nikajikuta kuishiwa na nguvu.Machozi yalianza
kuchururuzika kwa kasi nilijaribu kuyafuta kwa leso lakini bado haya
kukoma.Nilipitisha mkono kuhakikisha kwenye mpini wa bastola kuhakikisha
kwamba ipo.Nilipoigusa nikahisi ipo,nikaitoa na kuitizama kwa uchungu
sana.Nikasogeza risasi kwanye kifyatuo cha kuruhusu itoke,ilipoitikia
‘Katan’g..katan’g’Nilitikisa kichwa kwa fuhara ya kukusudia kufanya lile
nililofikiri kulifanya kwa wakati huo.Nilitembea kwa hadhari mpaka
dirishani walimo Getruda na Mzee Jophu.Nilijaribu kuchungulia lakini
sikufanikiwa kuona ndani kwakuwa kulikuwa na pazia nzito.Lakini kwa
kelele zile ,nilifikiri nikipiga risasi kwa kuhisi ningewaua kwa
pamoja.Nilipozidi kusikiliza kelele zao ,niligundua walikuwa karibu na
lile dirisha niliposimama.Niliuelekeza mdomo wa bastola yangu aina ya G3
rafles dirishani.Nikaingiza kidole ambacho nilitegemea kuwaulia .Kabla
sijafyatua risasi,nilishikwa mkono na mtu aliyekuwa nyuma yangu.
“Kaka usiwaue.Utajiingiza matatani bure.Nenda kapumzike nyumbani,hasira hasara kaka”
Mtu
huyo alinisihi akiwa ameing’ang’ania bastola.Kwanza aliniomba nitoe
risasi zote zilizomo ndani ya bastola.Nilipofikiri nikaona hakukuwa na
ulazima wa kubishana nae.Nilizitoa,akasema “Kaka naomba unipatie hizo
risasi .Najua unahasira unaweza kufanya lolote”Nilimpatia nikijua kama
ni kujiua basi naweza kutumia njia nyingine.Nilipompatia alizihifadhi
mfukloni mwake. Kila nilipofikiria, niliona kuwa sio suluhisho heri kufa
mimi kwa aibu niliondoka eneo lile, wahudumu walikusanyika wakinitazama
kwa huruma, wengine waliniomba niende niachane nao.
Waliendelea
kuvuta raha na wote waliyafurahia mapenzi yao, hasa Getruda aliamini
amepata mwanaume bora, ambaye asingemdhulumu haki ya unyumba. Alitumaini
na alitamani kuzaa na mzee Jophu ili kuondoa maneno ya mtaani kuwa ni
mgumba, alitegemea msaada mkubwa na juhudi za Mzee Jophu ili naye aitwe
mama.
Niliona Dunia chungu mithili ya shubira, kila nilipo kumbuka maneno ya Getruda na Mzee Jophu nilitamani nisitishe uhai wangu, sikuwa njia nyingine ya kuwepuka aibu ile, wakati na waza nafasi nyingine ilininyima kufanya uamuzi
huo na kunitaka niwe na subira. Niliamua kunywa pombe ili kupunguza
mawazo lakini mawazo yalizidi kutawala ubongo wangu kadri nilivyokunywa,
niliamua kusitisha kilevi, Sononeko liliendelea kunitawala, nikajiona
ni mtu dhaifu kuliko watu dhaifu wote duniani. Muda mwingine nilijaribu
kufariji kuwa ipo siku mungu atasikia kilio changu na kunipa nguvu za
ajabu,Maneno, “MUNGU UNAJUA MATESO YANGU” yakawa gumzo akilini kila
siku.
“Yaani
mke wangu ananidhalilisha kiasi hiki? Kweli yote haya ni kwasababu ya
udhaifu wangu,naamini mungu atasikia kilio cha mja wake na ataniponya
gonjwa hili na kunipa nguvu ili kuinusuru ndoa yangu
isivunjike”Niliongea huku nikiwa nimefumba macho, kichwa nikiwa
nimekiinamisha, kikiwa kina saidiwa kushikiliwa na viganja vya mikono.
Pamoja
na mawazo, hasira za kudhalilishwa. Bado nilikuwa na mpenda mke wangu,
nilimsubiri aje tukajipumzisha chumbani na kuongea utofauti
uliojitokeza. Kila nilipotizama saa ya ukutani,
niliona mshale kama unaenda mbele na kurudi nyuma, hali ile iliniadhiri
kisaikolojia. Nilikuwa nikiingia chumbani na kutoka, chooni na kutoka
bila kufanya chochote. Nilitamani kulala lakini sikupata hata tepe la
usingizi. Nilijikuta kutomlaumu tena mke wangu,kwani yote ni kwa sababu
sikuweza kumtimizia haki yake, nafsi nyingiune ilipinga na kusema
“Matendo aliyofanya ni ukosefu wa adabu na kutoheshimu unyumba, kwanini asifanye siri?”.Kila nilipokumbuka macho yalijaa machozi.
*****************
Ulikuwa
usiku wa saa sita na nusu, usiku mzito,Mwezi ukiwa umefunikwa na wingu
zito na ukungu mkubwa ukiwa mbele yake, mwili wake ulionekana kuchoka
mno!,akiwa anachechemea,mwendo ambao ulikuwa tofauti toka
kumuoa.Alinyanyua mkono sambamba na jiwe alilookota na kuanza kugonga
mlango kwa kishindo.Sikugonga tu pia kinywa chake kilipayuka maneno
machafu bila kujali alionitende.
“Wewe
mlinda nyumba umelala au upo macho?. Katika wasio na faida mmojawapo ni
wewe,wajanja wameondoa boma la mapenzi. Wewe unafananishwa na shoga,
mlinda nyumba. Funguaaaa”
Dharau
na maneno ya kashfa niliyasikia kwa usikivu wa masikio yote mawili,
maneno yalikuwa angali ya moto, nilihisi homa kali ikinitetemesha mwili,
nafsi ikakata tama ya kuishi kwa maisha ya manyanyaso, udhalilishaji na
matusi.
Nilifikiria
na kumfungulia mlango na kumuamuru aingie ndani, Getruda aliingia kwa
miondoko ya maringo huku akivumilia maumivu aliyoyasikia kwenye via vya
uzazi. Macho ya dharau yalinitizama kuanzia unyayo hadi kichwani na
kunipindulia midomo iliyojaa dharau kem! Kem!, hakuishia hapo alinisonya
na kutema mate pembeni, akijifanya anasikia kinyaa kunitizama.
“Mambo
baba wa nyumba”, akimaanisha mimi ni kama mlinzi wa kulinda nyumba,
sina mamlaka na penzi lake wala siwezi kutia neno kuhusu kuchelewa kwake
kufika nyumbani.
Niliitikia
salamu yake kwa shingo upande, sikupenda kumuudhi mke wangu, nilitambua
jinsi gani mtu anavyoumia pindi apatapo sononeko la roho. Kwa sauti ya
chini na ya upweke, hasira ikiwa imenikaba kooni.
“Mke
wangu umetoka wapi saa hizi, na ulikuwa unafanya nini?” Nilijizuia ili
mke wangu asijue kuwa nilikuwa na hasira, hata hivyo nilishindwa
kujizuia kulia, mwili mzima ulitetemeka, macho yakabadilika rangi kuwa
mekundu.
“Nimetoka
SEA BREEZ INN HOTEL kukagua mahesabu ya leo”. Getruda alijaribu kuongea
uwongo mtupu!, bila kupepesa macho, mboni wala kope za macho, macho
maangavu yasio na siri hata chembe.
“Nakubali
umetoka SEABREEZ INN, lakini sio kukagua mahesabu, bali umeenda kwa
mambo ya ufuska.” Hasira ilizidi kupanda kila nilipomtizama, mwili
ulizidi kutuna kwa hasira na jasho lilitoka kila sehemu yenye vitobo vya
vinyweleo mwilini.
“Hapana
mume wangu sikuwa nafanya ufuska” maneno yake yalinichanganya, nikaamua
kuchukua uamuzi ambao haukuwa akilini, niliamua kumuua mke wangu na
nilikuwa na sababu za kumuua, sikuwa tayari kutupiwa jicho na jamii kwa
udhaifu wangu.
Nilitoka
nilipokuwa, nikaingia ndani upesi, sikupenda kupoteza muda niliokota
jambia lenye makali kila upande, lenye kuwaka waka hata gizani,
nililitizama na kuamini kwamba ningelipitisha mara moja ningeachanisha
kichwa na kiwiliwili cha Getruda.
“Hakuna tena kumuuliza. Sio matangazo ya vifo.Nikifika ni kuachanisha kichwa chake”. Niliondoka nikimfuata alipo.
“Lazima nimuue Malaya huyu.Tukose wote, siwezi kujiua lazima nimuue leo leo”.
Nilipofungua
mlango, aliniona nikiwa na jambia lenye makali, aliamini kunusurika na
kifo ni asilimia mbili na zilobaki zilikuwa kifo, hapakuwa na upenyo
wowote wa kukimbilia kujinasua na mauti, “Haaaa!” Alihamaki na kujikuta anapiga kelele za kuomba msamaha.Ili nisitishe zoezi la kumuua bila mafanikio yoyote, sana sana niliongeza mwendo nikimfuata, jambia nikiwa nimeliinua juu tayari kutawanyisha shingo na kiwiliwili.
“Mume
wangu naomba unipe nafasi ya mwisho nikueleze yote yaliyotokea. Naomba
unisamehe usitoe uhai wangu, naamini utaridhika na matokeo. Kumbuka kuna
Mungu nae anayaona unayotaka kunifanyia” aliendelea kulia, akiomba
msamaha huku akirudi kinyume nyume taratibu.
Nilikusudia kumuua na sura yangu ilibadilika na kuonyesha dalili za kuua tu!, moyo wa huruma uliondoka; kwania ya
kumchinja kama kuku anavyochinjwa na kisu chenye makali. Nilizidi
kumfuata alivyokuwa anarudi nyuma, hasira ilitawala machoni. Ilikuwa si
rahisi kumsamehe kamwe!. Wakati Getruda anarudi
nyuma aliikwaa kwa nyuma na kudondoka chini kwa chali, hakuwa na njia
nyingine ya kujinasua na mauti, aliamua kusubiri mauti yamfike.
Nililikamata
jambia vizuri kwenye mpini wake kwa mikono miwili.Kitendo
chakutakakulishusha Getruda alishituka na kuzirai pale pale, aligeuza
macho, nilisitisha kumuua.Nilitaka kumuua akiwa na nguvu zake zote na
nilitaka afe kifo cha mateso.Nikaweka jambia pembeni na kuinama
kuhakikisha kama alizirai kweli ama ilikuwa janja ya
nyani.Niliposikilizia mapigo yake ya moyo yalikuwa mbali sana. Sikutaka kumpeleka hata hospitali nilitaka afe mwenyewe, si tena kumtibu, nilimchukia Getruda kwa mambo aliyonitendea.
Nililiokotajambia
langu nakulirudisha chumbani.Nilimuacha pale sakaruni akiwa kalala
chali.Nililitupa uvunguni kwa kitanda na kikajitupa kitandani kifudi
fudi. Muda mfupi usingizi ulinichukua, niliposhtuka ni ndege waliokuwa wakiimba
alifajiri. Niliamka na kufungua mlango waVarandani. Nilipochunguli
niliona bado Getruda alikuwa vile vile alivyodondoka usiku. Nilishindwa
kujua kuwa alikwisha kufa au laa!.Kwa vile nilikuwa mbali kidogo. Sikupenda hata kumsogelea, nilifunga mlango, nikakiendea kitanda kuendelea na usingizi.
Nikiwa
usingizini nilishituliwa na mlio wa simu, nilipoipokea nilisikia sauti
ya mwanaume na sauti hiyo haikuwa ngeni masikioni mwangu.
“ Hallo, vipi Bw. Sweedy?”alisema tu baada ya kusikianimepokea.
“Poa, nani unaongea”Nilimwuliza.
“Mimi Jophu, nauliza jana mkeo amerudi salama?”
Sikujibu kitu zaidi ya kuikata simu.
Baada ya saa moja hasira ilipungua, moyo wa huruma uliniingia, nilitoka na kumfuata Getruda alipo, hali
yake ilizidi kuwa mbaya, damu zilimtoka puani, mapovu mdomoni.
Nilimpigia simu mteja wangu Jangala aje nimpeleke Getruda hospitali,Kama
kawaida Jangala hachelewi alifika na tukampakiza Getruda.
“Vipi?.Mkeo ana matatizo gani?”Jangala aliniuliza wakati akifunga mlango wa nyuma alipo Getruda.
“Anasumbuliwa na shinikizo la damu”
“Oooo! Pole sana Bw, Kachenje”
“Nishapoa”
“Tunampeleka hospitali gani?”
“Naona tumpeleke Hospitali ya rufaa Mount Meru”
“Poa”Alijibu na kuondoa gari kwa kasi,huku likiwa limeacha vumbi zito nyuma.
Nilimfikisha
hospitali ya Mount Meru kwa matibabu. Aliingizwa chumba maalum cha
wagonjwa waliozidiwa ACU na muda mfupi aliwekewa mashine ya kumsaidia
kupumua. Walipomaliza walimtundikia maji ya mwili. Daktari walijitolea
kuokoa maisha ya Getruda kadri walivyoweza. Muda mfupi nikiwa kwenye
benchi, niliona mlango ukifunguliwa, alitoka nesi mmoja mwenye asili ya
kiarabu, kwa haraka nilijikuta moyo ukinipasuka. Nilimfananisha na
Jenifer niliyekutana nae nchini Thailand. Alinifuata pale nilipokuwa,
kitu kilichokuwa tofauti ni kwamba yeye alivaa magwanda meupe, “ Halo,
kaka wewe ndiye muuguzi wa Getruda Kimario?” nilishindwa kumjibu midomo
ilibaki wazi, niliamini kwa hali mbaya ya Getruda nesi aliniletea
taarifa mbaya.
“Kwani kuna nini nesi!…naomba unieleze!”niliongea mwili ukinitoka jasho pamoja na mambo mabaya Getruda aliyo nitendea lakini nilimpenda sana.
“Usiogope kaka. Niambie wewe ni muhusika?” Alisema tena kwa sauti ya chini.Nibaki nimeduwaa kama sekunde kadhaa.
“Ninani
kwako?”Aliuliza tena ,lakini safari hii alionekana kukasirika.
Nilishindwa kumwambi nilibaki machozi ya kinichuruzika, “Hata nikisema
ni mke wangu sijawahi kukutananae kimwili, sasa ni mwambie mimi ninani
wake?.Nikiwa nawaza, nikajikuta naropoka.
“Ni dada yangu” niliongopa
“Ok, pole sana mungu
amemsaidia. Sasa ananafuu”akatulia kidogo na kunitupia tabasamu pana
lililoshiba midomoni mwake.Kisha akasema “Tunategemea kumpa ruhusa
kesho. Mungu akipenda”Nilipandisha pumzi na kuishusha kwa
nguvu”oooophhhh!” nikajifuta jasho.
Kesho yake Getruda aliruhusiwa kurudi nyumbani.
No comments:
Post a Comment