Artikel Terbaru

Responsive Ads Here

Saturday, April 29, 2017

JINSI YA KUPANGA UZAZI KWA MWANAUME KWA NJIA YA UPASUAJI{VASECTOMY]…




                                                

Habari za zenu ndugu wasomaji, natumaini mnaendelea na shughuli zenu za kila siku kama kawaida.
Katika mtiririko wetu wa makala za uzazi wa mpango, leo tutaongelea uzazi wa mpango kwa mwanaume.
Watu wengi hua hawajui kama mwanaume pia anahusika pia kufungwa mirija kama ilivyo mwanamke ili asiweze kumpa mimba mwanamke tena na baada ya hapo kuishi maisha ya kawaida kabisa..
Njia hii ni imekua ngumu kidogo kupokelewa kwa tamaduni za kiafrika labda kwa sababu ya imani zilizopo na wanaume kutoathirika moja kwa moja na tatizo la kubeba mimba nyingi..
Jinsi ya kufanya upasuaji..
Upasuaji huu hufanyika kwenye korodani na mirija inayopeleka mbegu za kiume kutoka kwenye korodani kwenda kwenye uume kitaalamu kama vas deferens hukatwa kabisa kuzuia mfumo huo wa uzazi..
Mwanaume huweza kuendelea na shughuli zake za kawaida baada ya wiki moja tu.
Madhara ya njia hii ya uzazi wa mpango..
Yapo madhara madogo madogo ya njia hii ya uzazi wa mpango kama kutokwa na damu, maumivu, na kidonda kuchelewa kupona kwasababu ya kuingiliwa na bacteria{ infection}.
Lakini madhara haya haya huweza kutibika kirahisi sana..
Baada ya upasuaji
Upasuaji huu ni wa moja kwa moja yaani hautaweza kumpa kwanamke mimba tena hivyo ni vizuri kua na uhakika kabla hujaamua kushiriki njia hii,
Ni nchi chache zilizoendelea zilizofanikiwa kurudisha mirija hiyo tena lakini bado uwezekano wa kumpa mwanamke mimba unakua chini yaasilimia 55.
Mwisho; hii ni moja ya njia bora za uzazi wa mpango ambazo hazina madhara kabisa kiafya na huweza kutumika mda na wakati wowote muhusika anapokua tayari.

No comments:

Post a Comment